Skip to main content

UGONJWA WA KUANGUKA KIFAFA

Naam! Mpendwa msomaji wa blog yangu hii habari za saa hizi, nimatumaini yangu u mzima wa afya njema. Napenda kutumia nafasi hii kukupatia japo kidogo habari ya ugonjwa wa kuanguka kifafa.

Inakadiliwa kuwa kwenye nchi zinazoendelea asilimia moja ya watu wake wana ugonjwa wa kuanguka kifafa. Kati ya watu hao nusu yao ni watoto na hali hiyo inaweza kudumu maisha kama haikutibiwa.

Kwenye nchi hizi wagonjwa wa kuanguka kifafa hudhalilishwa na hivyo kutengwa na jamii kwani ugonjwa huu hudhaniwa kuwa ni wa kuambukizwa.

Kwa hiyo wagojwa hawa hula na kucheza peke yao na hivyo hawaruhusiwi kujiunga na wenzao katika kazi na shughuli nyingine za kijamii ingawa akili zao mara nyingi zipo sawa kabisa.

Hivyo baada ya kusoma makala haya utaweza kuelewa baadhi ya mambo muhimu kuhusu ugonjwa wa kuanguka kifafa na kwamba ugonjwa huu HAUAMBUKIZI.

UGONJWA WA KUANGUKA KIFAFA NI NINI?

Ugonjwa wa kuanguka kifafa ni ugonjwa unaoathiri ubongo. Ugonjwa huu huwakumba watu wa aina na mataifa yote hapa ulimwenguni bila kujali dini, rangi, kabila au kiwango cha elimu yao.

Hali ya kuanguka kifafa inaweza ikaanza wakati wowote, lakini mara nyingi hujitokeza wakati wa utotoni. Mtu aliyepatwa na ugonjwa huu huanguka na kujitupatupa kiwiliwili chake, kujiuma ulimi, na hatimaye kupoteza fahamu. Akiwa amepoteza fahamu anaweza kujikojolea pia.

Ni vyema kuelewa pia kuwa mtu mwenye kuanguka kifafa hawezi kuambukiza mtu mwingine ugonjwa huu kwa njia ya:

a. Kutoa ushuzi

b. Pumzi

c. Mkojo

d. Haja kubwa

e. Kugusana

f. Jasho

g. Kutumia vyombo vya chakula pamoja.

KUANGUKA KIFAFA KUNASABAIBISHWA NA NINI?

Sababu kuu za kupatwa na ugonjwa wa kuanguka kifafa ni kupata;

: athari kwenye ubongo wakati mama anapokuwa na uzazi wa matatizo au uzazi wa muda mrefu,

: magonjwa yanayaoathiri ubongo kama vile malaria na ugonjwa wa uti wa mgongo,

: majeraha kichwani yanayotokana na ajali ya gari, kupigwa, matumizi ya Pombe kali kwa muda mrefu au uvimbe kwenye ubongo.

MATIBABU YA UGONJWA WA KUANGUKA KIFAFA

Ugonjwa wa kuanguka kifafa unatibika ili mradi tu mgonjwa anafuata maagizo ya matumizi ya dawa kama anavyoelekezwa na mganga wake. Kuna dawa nyingi zinazotumika kutibu ugonjwa huu, kati ya hizo ni ‘Phenobarbitone’na ‘Phenytoin’ Iwapo mgonjwa ataandikiwa mojawapo ya dawa hizi ni lazima zimezwe kufuatana na maagizo ya Mganga na kwa kufanya hivyo tu ndipo vipindi vya kuanguka vitapungua.

KUMBUKA: MTU MWENYE KUANGUKA KIFAFA SIYO MGONJWA WA AKILI, MHALIFU, KWAMBA ANA MASHETANI AU MWAMBUKIZAJI.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...