Skip to main content

ASASI NYINGI NCHINI ZIMO HATARINI KUFA



MASHIRIKA yasiyokuwa ya kiserikali (NGOs) yamo hatarini kufunga milango ya ofisi zao kutokana na viongozi wengi wa mashirika hayo kukosa kabisa utaalamu wa kuandika miradi mbalimbali kwa ajili ya huduma za kijamii na badala yake yanasubiri wafadhili wenyewe wajitokeze jambo ambalo ni gumu sana kwa wafadhili kufanya hivyo imefahamika.

Hayo yalijitokeza jana katika semina ya siku tano ya kuwajengea uwezo viongozi wa mashirika hayo yasiyo ya kiserikali wilayani Ludewa iliyofanyika katika ukumbi wa MTC Mlangali na kuandaliwa na Ludewa Non Governmental Umbrella (LUNGOU) chini ya ufadhili wa The Foundation for civil society ya jijini Dar es salaam.

Pamoja na kuyajengea uwezo mashirika hayo juu ya uandaaji na uandishi wa miradi ya kijamii LUNGOU pia ili iliendesha semina ya ufahamu juu ya utawala bora ndani ya mashirika hayo na katika watumishi na wafanyakazi na watendaji ndani ya serikali na vyombo vya umma.

Akifungua semina hiyo Afisa maendeleo ya jamii wilayani Ludewa Bw. William Malima aliwataka viongozi hao wa mashirika yasiyo ya kiserikali kuacha tabia ya kusubiri wafadhiri waje kuwatafuta badala yake wayatumie mafunzo hayo kuwajengea uwezo wa kuandaa na kuandika wenyewe miradi ili kuwashawishi wafadhili kutoa fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali.

Bw. Malima alisema asasi nyingi za kiraia nchini zinakosa pesa kutokana na kutofahamu namna ya kundika maandiko ya miradi (project write up)hata zile chache zinazopata fedha bado zinakabiliwa na tatizo la utawala bora. Utawala bora ni pamoja na jinsi asasi inavyoendeshwa shughuli zake kwa njia ya vikao hasa kwa kukosa uwazi (Transparency) na uwajibikaji yaani (Accountability).

“Ndugu washiriki wa semina kuna umuhimu mkubwa wa kuandika miradi/maandiko ambayo malengo yake ni pamoja na kupata raslimali fedha, rasrimali mitambo (mashine) na vitendea kazi, rasriamali watu wenye ujuzi kama wataalamu ambao leo watatoa mafunzo namna ya kutayarisha na kushawishi wafadhili,”alisema Bw Malima.

Aidha, mgeni rasmi alisema asasi nyingi hushindwa kuandika miradi kwa kutojua ni miradi gani waandike, wakati gani na wapi wapeleke lakini wanasahau kuwa kwa sasa dunia inakabiliwa na matatizo kama ugonjwa wa Ukimwi, Umaskini uliokithiri hasa wa kipato, Uharibifu wa mazingira,Ukosefu wa utawala bora na Ukiukwaji wa haki za binadamu n.k.

Bw. Malima aliwataka washiriki na wadau wengine kwenda kuwaelimisha na kuhamasisha jamii, taasisi na vikundi viweze kuanzisha na kusajili asasi kwani katika Wilaya nzima ya Ludewa kuna asasi 38 tu zilizo hai wakati Tanzania yote hadi 2010 kulikuwa na asasi 6,000 idadi ambayo ni ndogo sana ukilinganisha na nchi ya Ufaransa yenye asasi 80,000 hadi sasa.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi Bw. Emanuel Kayombo mwenyekiti wa mwavuli wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali wilayani Ludewa aliwataka washiriki wa semina kushiriki vikamilifu mafunzo hayo kwani ndiyo ukombozi na uhai wa mashirika yao ama sivyo mashirika hayo yamohatarini kufutiwa usajili.

Bw. Kayombo aliwataka wanachama hao wa mtandao (LUNGOU) kutoa viingilio na michango yao ya kila mwaka ili kuweza kupata fedha za kuendeshea ofisi, na kuwataka viongozi ambao hawajasajili asasi zao kwa mwavuli wa mashirika ili kujua shughuli wanazofanya nia ikiwa ni kuepusha migongano ya kuandika miradi inayofanana kwa wafadhili na huduma zinazofanana.

Mkufunzi wa mafunzo hayo na mtaalam wa maandiko Bw Elwin Mligo kutoka Njombe aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kuwa makini katika kuandika miradi hasa kutokuchanganya Dira ya shirika, Dhima na Maadili sanjari na kuzingatia mfumo wa mti wa matatizo, mti wa malengo, bo la mantiki na Bajeti bila kusahau visababishi,matatizo na madhara.

Mafunzo yaliyotolewa katika semina hiyo ni pamoja na upangaji na usimamizi wa miradi, uchambuzi wa ndani na nje ya azaki, uchambuzi wa wadau na tathmini ya mahitaji, utayarishaji wa malengo yenye kuzingatia matokeo, kupanga bajeti ya mradi uchambuzi na umuhimu wake, tathmini na ufuatiliaji,viashiria na utawala bora.

Hata hivyo, washiriki wa mafunzo hayo waliomba shirika la The Foundation For Civil society lilifadhili mafunzo hayo kuongeza ufadhili mwingine kwenye mwavuli wao ili kuweza kukamilisha mafunzo hayo kwani muda uliotumika hautishi kumaliza masomo yote jambo lililofanya kukatisha kutokana na ufinyu wa bajeti yenyewe.





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...