Skip to main content

MAFISADI WATESA KWA ZAMU!

Na Gustav Chahe, Iringa


Jumla ya watuhumiwa wanane (8) ambao walitakiwa kupelekwa mahakamani kwa sababu za ubadhilifu wa pesa za mradi wa kijiji cha Madege umeingia dosari na wanakijiji kuutupia uongozi lawama za kushindwa kufanya hivyo. Zaidi ya shilingi milioni ishirini na moja (21m/-) za mradi huo ambao unaendeshwa kwa ufadhili wa Districts Agricultural Development Programme Support (DADS), yaani mpango wa kilimo wilayani, kutoka Denmark ulitiwa dosari na baadhi ya wanakijiji walioamua kujinyakulia fedha kinyemela na kuzitia mifukoni mwao.

Kijiji hicho kilipata bahati ya ufadhili wa mashine mbili zenye vinu vya kukoboa na kusaga kwa ajili ya maendeleo ya kijiji hicho licha ya kuwa kinakabiliwa na changamoto mbalimbali za kila aina ambazo zinahitaji nguvu kubwa itumike ili kujikwamua nazo.

Hasara hiyo inatokana na usimamizi mbovu wa wale waliopewa dhamana na kijiji kusimamia ikiwa ni pamoja na kutokuwa na na mwongozo wa uendeshaji na kuzitumia mashine hizo kama mali zao binafsi kwa ajili ya maslahi yao. Kwa kutochukuliwa hatua yoyote watuhumiwa hao kunatokana na ama kula njama moja na viongozi hao au kwa kile kinachosadikiwa na wengi kuwa ni hali ya kulindana ili kuepusha kuumbuana pindi watakapo kuwa kizimbani kwa ajili ya kutolea maelezo juu ya ubadhilifu huo. Itakumbukwa kuwa mmoja wa watuhumiwa alipohojiwa na mwandishi hapo katika makala ya awali alieleza kuwa haogopi kwenda mahakamani kwa kuwa kule ndiko atakakotolea maelezo ya ukweli na uhakika.

Bw. Elenasi Kikoti ambaye ni miongoni mwa watuhumiwa alidiriki kusema hivyo kwa mwandishi kwa kile alichosema hawezi kumwambia mtu yeyote siri aliyo nayo hadi kitakapoeleweka mahakamani hiko kwani akiongea mapema anaweza akageuziwa ubaya. “Ukweli mwandishi mimi siwezi ni katoa siri niliyonayo sasa hivi ili tutakapofika mahakamani ndiko nitakako toa siri yangu na kuzungumza ukweli kutokana na mambo ninayoyajua kuhusiana na mradi huu na mengine ambayo si ya mradi huu, lakini yanahusiana na maendeleo ya kijiji” alisema Bw. Kikoti.
Kwa mujibu wa ripoti ya tume iliyoundwa kwa ajili ya uchunguzi wa mradi huo, lilikuwa na orodha ya watuhumiwa ambao wanahusika moja kwa moja kujibu tuhuma na kustahili uadabishwa juu ya ubadhilifu wa pesa hizo. Ripoti hiyo imeorodheshwa majina ya Santina Msuva, Zamda Mtenga, Waride Sechambo, Elenasi Kikoti, Jasimini Kikoti pamoja na Boazi Kadinda, Athumani Kisima na Elisha Mhile. Mradi huo ulianza tangu mwaka 2006 ambao ulilenga kukinufaisha kijiji hicho chenye wakazi 2,225 pamoja na maeneo jirani ambao hutegemea kilimo katika kujipatia mahitaji yao ya kila siku na kuwajibika katika shughuli mbalimbali za maendeleo yao binafsi, kijiji hata kwa ajili ya maendeleo ya kitaifa kwa ujumla.

Aidha, Lesamu Msuva naye anaingizwa katika tuhuma hizo kwa kushindwa kuwajibika katika tatizo hilo wakati wa uongozi wake alipokuwa Diwani katika Kata hiyo katika kipindi cha awamu ya kwanza ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete. Mheshimiwa huyo anaingizwa katika kundi hilo kwa kile kinachodaiwa ufisadi kwake lilikuwa ni jambo la kawaida kwani aliogopa kuwakoromea wenzake kwa kuwa hata yeye wanakula sahani moja. Kama isemwavyo “mtoto umleavyo, ndivyo akuavyo”, kutokumuadabisha fisadi ni kuna maanisha kuwa hali hii ni ya kawaida kwa kuwa hakuna aliye safi wa kumuondoa mwenzake au wa kumkaripia na kumchukulia hatua. Hii ni kwa sababu ya usemi usemwao “ndege wenye mabawa yanayofanana, huruka pamoja”, ndivyo ilivyo hata kwa watu wa namna hiyo kulindana kwa ili wasiumbuane, lakini pindi inapotokea mmoja ameumbuka huwa inakuwa tafrani kubwa kwa maswahiba hao.

Awali akiongea na mwandishi wa habari hizi, Afisa Mtendaji wa kijiji hicho Bw. Elijus Kikoti alisema kuwa watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote utaratibu utakapokuwa umekamilika. Kadiri siku zinavyozidi kwenda hali ya kijiji inazidi kuwa mbaya kutokana na watu kutojitokeza kwa uwingi katika kutumia nguvu zao katika maendeleo ya kijiji hususani katika michango, na kujitoa pale wanapotakiwa kutumia nguvu zao.

Ikiwa viongozi wa kijiji hicho walikanusha madai ya wanakijiji kuwepo na hali ya kuogopana na viongozi kula sambamba na watu wanaotia hasara maendeleo ya kijiji hicho, hali inazidi kuonekana wazi kwa tuhuma hizo. Kiongozi mmoja ambaye jina tunalo, alipohojiwa na mwandishi wa makala haya juu ya kujihusisha na wanaosadikiwa kuwa ni wabadhilifu wa miradi ya maendeleo ya kijiji, alieleza kuwa wao hawatakuwa wa kwanza kujihusisha na watu kama hao wakati wapo wengi wanaofanya hivyo. “Siwezi kukubali au kukata, watanzania wa leo siyo wajinga kiasi kwamba wanaweza kudanganywa kirahisi. Najua watakuwa wanaongea wanachokijua. Kama ni hivyo, hatutakuwa wa kwanza sisi kufanya hivyo kwa sababu hata ukiangalia jinsi nchi inavyokwenda tunasikia kabisa hata ngazi za juu wanafanya hivyo sembuse na sisi ambaye ni wadogo kabisa. Kumbuka mwandishi kuna usemi ambao husemwa “mtoto wa nyoka ni nyoka tu” alieleza kiongozi huyo.

Kiongozi huyo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe alieleza waziwazi kuwa mpango huo kautatimia endapo safu ya uongozi uliopo haitafanyiwa marekebisho kwani haiwezekani watu wanaokula pamoja wakatafutana ubaya. “Ninaomba unilinde jina langu ili nikwambie ukweli. Ninakwambia, kama watuhumiwa hawa watapelekwa mahakamani tutaona. Ninasema hivi kwa sababu ninajua; miongoni mwetu tunakula sahani moja na watuhumiwa kwa hiyo mpango wa kuwapeleka watuhumiwa mahakamani utabaki maneno tu hadi utakapopotea tu hewani kwa sababu si rahisi wakafanya usaliti wanaoijua siri yote” alisema.

Mpango wa kuwapeleka watuhumiwa wa ubadhilifu wa fedha za mradi wa DADS wa kijiji cha Madege mahakamani umeota mabawa na kuwaacha watuhumiwa wakitesa kwa zamu kijijini hapo kwa raha zao. Watuhumiwa hao imeshindikana kupelekwa mahakamani kutokana na udhaifu wa uongozi wa kijiji hicho kuingiza udugu na urafiki badala ya kuwajibika katika nafasi zao za kiutendaji katika kuwahudumia wananchi.

Awali wananchi waliilalamikia serikali ya kijiji hicho kuwachukulia watuhumiwa kama ndugu zao na kuwakingia kifua ili suala liweze kupotea bila maelezo na kuwaacha wananchi gizani bila kujua kinachoendelea. Mradi huo ulitiwa dosari na baadhi ya wanakijiji hicho walioamua kujinyakulia fedha kinyemela na kuzisweka wanakokujua wao na kuwaacha wanakijiji wakihaha bila kupata majibu huku wakipoteza nguvu zao kwa ajili ya maendeleo ya kijiji.

Itakumbukwa awali wananchi walidai kuwepo na hali ya kubebana ambako ni sababu kubwa inayosababisha kutowafikisha watuhumiwa hao mahakamani. Maelezo ya viongozi wa kijiji yalionekana kwenda tofauti na kauli za wananchi kwa kile walichokieleza kuwa hawezi kumuogopa mtu yeyote kwa namna yoyote ile. Hali inazidi kuwa mbaya kutokana na mashine hizo kusimama badala ya kuhudumia wanakijiji huku wanakijiji wakibaki na mahangaiko yasiyokuwa na majibu na viongozi wao wakiendelea kubaki kimya. Bado wanakijiji wanaendelea kulalamika ili haki iweze kutendeka na sheria iweze kuchukua mkondo wake dhidi ya watuhumiwa hao vinginevyo hali si shwari. Wakizungumza na mwandishi wa makala haya kwa nyakati tofauti, wanakijiji wanaulalamikia uongozi wa kijiji hicho kuwa wanafanya kazi kwa upendeleo huku wengine wakiumia kwa ajili ya maendekeo ya kijiji. “Ndugu mwandishi, sisi wanakijiji tupo gizani hadi sasa kuona viongozi wetu wanakaa kimya bila kutuelekeza ni nini kinaendelea kwa watuhumiwa hao wanaotutesa sisi wengine” anasema mwanakijiji mmoja.

Pia anasema ni bora kutolea maelezo kama wanashindwa badala ya kukaa kimya kwani wapo wanakijiji ambao wanaweza wakalifanya hilo kwa ufanisi kulingana na uchungu wao kwa kijiji na nguvu zao wanazozipoteza kwa ajili ya maendeleo ya kijiji hicho. “Kama wanashindwa kufanya kazi na kuwapeleka watuhumiwa hao mahakamani watueleze ili sisi wanakijiji tujue la kufanya; tunaweza tukawateua watu ambao tunawaamini walisimamie suala hilo kuwapeleka mahakamani” anasema mwanakijiji huyo.

Naye katibu wa kamati ya uchunguzi wa mradi huo Bw. Felix Kayage anaeleza kuwa, tatizo ni porojo nyingi kuliko uwajibikaji na ndiyo maana maendeleo ya kijiji yanazidi kudumaa. “Ukweli ni kwamba porojo ni nyinyi kuliko uwajibikaji na ndiyo maana tunashindwa kufanya kazi za msingi; kama uwajibikaji ungekuwa wa kifanisi, watu kama hao wasingekuwa wanafumbiwa macho kwa muda wote huo na kusabasha hasara kuendelea kujitokeza zaidi” anasema Bw. Kayage. Taarifa za kuaminika zilizolifika gazeti hili zinasema, moja ya mambo ambayo yanakwamisha maendeleo katika kijiji hicho ni kuwepo kwa undugu zaidi kuliko uwajibikaji wa viongozi katika nafasi zao kwa kutenda haki. “Ndugu mwandishi, hiki kijiji hakiwezi kuendelea kamwe kutokana na viongozi kuendekeza undugu na urafiki badala ya kuwajibika katika nafasi zao. Tabia hii ndiyo inayotumaliza sisi wananchi kila kunapokucha kwa kuwa hata anayeonekana kwenda kinyume na utaratibu wetu akiowa ni rafiki wa kiongozi au ndugu wa kiongozi, hawezi kuadabishwa” kinasema chanzo hicho. Katika maelezo ya wanakijiji waliowengi, wanakijiji wanazidi kukata tamaa siku hadi siku kutokana udhaifu walionao viongozi wao kiutendaji na kuwajibika katika malalamiko na ushauri wao kwa ajili ya ufanisi bora.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...