Skip to main content

MEI MOSI WAFANYAKAZI LUDEWA WAKERWA NA KIBURI NA KEJELI...



.Waajiri na Wakuu wa idara wakwepa kujitokeza kwenye sherehe hizo.



MAADHIMISHO ya sherehe za mei mosi yanayofanyika kila mwaka duniani kote yamewachefua wafanyakazi nchini hususani Wilayani Ludewa kutokana na viongozi na baadhi ya wakuu wa idara kupuuza na kuchelewesha maslahi na stahili za wafanyakazi wa kada za chini.

Akisoma risala kwa niaba ya wafanyakazi wote mwenyekiti wa shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi Wilayani Ludewa Mkoani Njombe Bw Joseph Thomas Mvanga alisema waajili wanakatisha tamaa wafanyakazi wao na kusababisha kufanyakazi chini ya kiwango.

Bw Mvanga alizitaja kero hizo kuwa ni pamoja na kuchelewesha mishahara yao ya kila mwezi, kutopandishwa vyeo kwa wakati, mazingira mabaya ya kufanyia kazi, viongozi na waajili kutoa lugha chafu na kejeli kwa wafanyakazi wa kada ya chini, wastaafu kucheleweshewa mafao yao kunapelekea wastaafu waatarajiwa kukata tama na kuingiwa na hofu kila wanapokaribia kustaafu hasa wanapoona mateso wanayopata waliotangulia.

Naye mwenyekiti wa chama cha walimu (CWT) Wilaya ya Ludewa mwalimu William Kunyanja Akimkarisha mgeni rasmi Bw John Mahali ambaye ni katibu tawala wilaya ya Ludewa alisema kero za wafanyakazi zitatuliwe kwa ushirikiano ili kuondoa wasiwasi na kujenga uaminifu baina ya mwajiri na mwajiriwa.

“Inasikitisha sana kuona kila mwaka mei mosi wafanyakazi wanawasilisha kero na malalamiko yao lakini serikali imeziba masikio kama vile haisikii hii inaondoa maana ya maadhimisho haya kwa sababu matatizo kila mwaka tunatoa kero lakini hazitekelezwi”” alilalamika Bw Kunyanja

Alimwambia mgeni rasmi kuwa kupuuzia kunakofanywa na waajili kunaongeza msongo wa mawazo na mheuko kwa watumishi wenye uhitaji wa huduma kutoka kwa viongozi wao na kuitaka serikali kuchukua hatua na kushughulikia kero kwa wakati bila mizengwe na kwamba kwa kufanya hivyo rushwa na uzembe kazini vitakwisha.

Akijibu risala hiyo ya watumishi Bw John Mahali katibu tawala wa wilaya ya Ludewa (DAS)ambaye alimwakilisha Mkuu wa wilaya hiyo aliyekwenda kuhudhria maadhimisho ya mei iliyofanyika kimkoa wilayani mfindi alikiri kuzitambua kero hizo na kusema kuwa zinahitaji ushirikiano katika kuzitatua.

Hata hivyo aliahidi kuzishughulikia kero hizo lakini akawaambia waajili na wakuu wa idara wachache waliohudhuria sherehe hiyo kuwa mei mosi ijayo wawe wamezishughulikia kero hizo. Na kwamba siyo busara kila mwaka wafanyakazi kulalamikia mambo yaleyale.

Hata hivyo Bw Mahali alisikitishwa na tabia mbaya iliyooneshwa na wakuu wa idara katika Halmashauri hiyo na waajili kwa kutohudhuria na kutoshiriki vyema katika viwanja yalipofanyika maadhimisho ya sherehe hizo za mei mosi zilizofanyika kiwilaya katika kata ya Ludewa.

“Katika sherehe kama hizi inatakiwa wakuu wa idara na waajili wawepo wenyewe hapa na kusikiliza kero za watumishi waliochini yao kwa sababu yapo mambo yanayowahusu wao na matatizo mengi yapo chini ya uwezo wao kwa sababu wao ndio wanaoshinda na watumishi hao.” Alisema Bw Mahali

Hata hivyo aliwaagiza waandaaji wa maadhimisho hayo kuwashirikisha waajili wengine wa kutoka katika sekta binafsi kwa sababu mfanyakazi siyo wa serikalini tu na kwamba siyo vizuri kuwatenga watu binafsi na kuwataka waajili kuacha tabia ya kusema njoo kesho hiyo hali imepitwa na wakati.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...