Skip to main content

RAIS KIKWETE MGENI RASMI KATIKA KUMSIMIKA ASKOFU NDIMBO

ASKOFU MTEULE WA JIMBO LA MBINGA
MHASHAMU JOHN C. NDIMBO





RAIS Jakaya Mrisho Kikwete anatarajia kuwa mgeni rasmi katika sherehe za kumsimika Askofu Mpya wa Pili wa Jimbo Katoliki la Mbinga mkoani Ruvuma hapo tarehe 05.06.2011. Aidha, Ibada ya kuwekwa wakfu Askofu huyo itaongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Da es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.

Akiongea na Blog ya http://www.fridaysimbaya.blogspot.com/ leo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Jimbo la Mbinga Pd. Jospeh Mwingira amesema kuwa Rais Kikwete ndiye atakuwa mgeni rasmi katika sherehe za kumsimika rasmi na kuweka wakfu Askofu Mteule wa Jimbo la Mbinga, Mhashamu John Chrisostom Ndimbo.

Jimbo Katoliki la Mbinga limepata Askofu Mpya aliyeteuliwa na Baba Mtakatifu Benedikto XVI kuwa Askofu wa Pili wa Jimbo hilo. Mwashamu Askofu John Ndimbo aliteuliwa na Baba Mtakatifu Benedikto XVI kuwa Askofu wa pili wa Jimbo Katoliki la Mbinga hapo tarehe 12 Machi, 2011.
Uteuzi huo umefuatia kustaafu kisheria kwa Mhashamu Askofu Emmanuel Mapunda aliyeliongoza jimbo hilo kwa miaka 21 mpaka sasa. Mhashamu Askofu Emmanuel Mapunda amefikisha umri wa miaka 75 ambayo kwa taratibu na sheria za Kanisa Katoliki, maaskofu wake wafikapo umri huo wanapaswa kustaafu majukumu ya kuliongoza jimbo.

Askofu Mapunda alifikisha umri huo tarehe 10. 12. 2010. Baada ya kupeleka maombi ya kustaafu kwa mkubwa wake Papa Benedikto XVI, Askofu huyo alikubaliwa na kuomba aendelee kusimamia Jimbo la Mbinga hadi hapo Askofu mpya atakapoteuliwa.
Askofu Jonh C. Ndimbo alizaliwa tarehe 12. 10. 1960 huko Kipololo katika Parokia ya Lundamato Jimbo la Mbinga. Wazazi wake walikuwa Chrisostom Ndimbo na Fransiska Ndunguru. Ubatizo alipata tarehe 13.11 1960 na kipaimara tarhe 29.10. 1972.

Shule ya msingi alisomo huko Kipololo katika Porakia ya Lundamato la Jimbo la Mbinga, kwa darasa la kwanza hadi nne mwaka 1969 hadi 1972. Masomo ya darasa la tano hadi saba alisoma huko Hanga Seminari katika Jimbo Kuu la Songea kuanzia mwaka 1973 hadi 1975.

Masomo ya sekondari alisoma katika Seminari za Likonde katika Jimbo la Mbinga (wakati huo lilikuwa Jimbo la Songea) na Nyegezi katika Jimbo la Mwanza. Kidato cha kwanza hadi cha nne mwaka 1976 hadi 1979 huko Likonde. Kidato cha tano hadi cha sita mwaka 1980 hadi 1981 huko Nyegezi.

Pia alipata mafunzo ya kijeshi huko Urujoro-Arusha maka 1982. Kisha aliendelea na malezi na kozi ya upadre katika Seminari Kuu Peramiho. Falsafa alisoma mwaka 1983 hadi 1985 na teolojia mwaka 1986 mpaka 1989. Alipewa Daraja Takatifu la Ushemasi Juni 1988 na upadre 21.06. 1989 huko Mbinga na Mhashamu Askofu Emmanuel A. Mapunda wa Jimbo la Mbinga. Yeye ni miongoni mwa mapadre sita (6) waliopadrishwa mwaka huo jimboni Mbinga.

Baada ya upadrisho Pd. John Ndimbo alitumwa seminari ya Likonde kuwa mwalimu na mlezi wa waseminari. Mwaka 1990 alipelekwa Ufilipino kwa masomo ya juu ambako alipata shahada ya kwanza na ya pili katika masomo ya sayansi na utawala wa elimu. Vyuo alivyosoma ni Rigina Carm Katikaeli kilichopo katika jiji la Manila na cha DE LA SALLE hapa hapo Manila. Alihitimu masomo hayo mwaka 1994 na kurudi jimboni Mbinga.

Tarehe 8 Septemba 1994 aliteuliwa na Mhashamu Askofu Emmanuel Mapunda kuwa Gombera wa seminari Likonde wadhifa aliodumu nao mpaka tarehe 28. 09.2010 alipoacha kufuatia kuteuliwa kwake kuwa Katibu Mtendaji wa Idara ya Elimu ya Baraza la Maaskofu Tanzania tarehe 3 Agosti 2010.

Mhashamu Askofu John Ndimbo ni Askofu pacha wa Mhashamu Askofu Bernadine Mfumbusa wa Jimbo Katoliki la Kondoa katika Mkoa wa Dodoma. Kwani, siku alipoteuliwa na kutangazwa Askofu John Ndimbo wa Jimbo la Mbinga, tarehe 12 Machi, 2010, Baba Mtakatifu Benedikto XVI alianzisha Jimbo la jipya la Kondoa lililozaliwa kutoka Jimbo la Katoliki la Dodoma. Kisha akamteua Pd. Bernadine Mfumbusa, ambaye alikuwa makamu  mkuu wa taaluma katika chuo kikuu cha Kanisa Katoliki cha Mt. Augustino (SAUTI) Mwanza .

“Jimbo jipya la Kondoa lina eneo la kilometa za mraba 13, 210, watu 541,345, wakatoliki 46,067, mapadre 17, watawa 87. kumbe, Jimbo Katoliki la Mbinga ambalo lina milikiwa na Mhashamu Askofu John Ndimbo lina eneo la kilometa za mraba 11, 400, watu 532,019, wakatoliki 418,000, mapadre 69 na watawa 270,” sehemu ya taarifa inaelezea.

Uteuzi wa maaskofu hawa umepokelewa na wakristo na Watanzaia kwa ujumla kwa hisia za pekee na tofauti. Kundi kubwa la watu linasifu na kupongeza uteuzi wao, lakini wengine wanaonja kwa karibu sana pengo waliloacha katika nafasi zao walizoziacaha. Wote hao wamekuwa katika nafasi za juu na nyeti za kitaaluma katika Kanisa letu.

Mhashamu John Ndimbo alikuwa Katibu Mtendaji wa Idara ya Elimu TEC baada ya kushughulika na taaluma kwa miaka 22 katika seminari Likonde, hivyo kwa uhakika ana mang’amuzi na uzoefu wakutosha.

Mhashamu Askofu Mfumbusa amekuwa makamu wa mkuu wa taaluma katika chuo cha SAUTI-Mwanza na mhadhiri nguri wanafunzi wa kozi ya uandshi wa habari. Hapo alikuwa mhimili mkubwa wa taaluma ya mwasiliano.

Wahashamu maaskofu Benedine Mfumbusa na John Ndimbo walikula kiapo cha utii na kukiri kanuni ya Imani kwa kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki Papa Benedikto XVI huko Roma katika Kikanisa cha mweyeheri Kardinali Henry Newman hapo tarehe 4 Aprili, 2011. Katika nafasi hiyo walikabidhiwa vitendea kazi vya kiaskofu.

"Tunawatakia maaskofu wetu hawa amani, baraka na nguvu katika wajibu huo mpya. Mungu aandamane nao daima."



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...