Skip to main content

SIKU YA MALARIA DUNIANI IMANI ZA KISHIRIKINA ZA CHANGIA KUONGEZEKA KWA VIFO

Na Friday Simbaya, Ludewa
WAKATI Taifa likishehekea mafanikio ya kuudhibiti ugonjwa hatari wa Maralia kwa kugawa vyandarua kwa mama wajawazito na watoto walio na umri chini ya miaka mitano Mkoani Iringa bado vyandarua havitoshi, lakini vilivyopo vinatumika kujifunika kama blanketi kujikinga na baridi imefahamika.

Hayo yalithibitika hivi karibuni katika kijiji cha Mbwila Kata ya Luana Ludewa Mkoani Iringa wakati wa maadhimisho ya siku ya malaria kimkoa ambapo mkuu wa wilaya ya Ludewa Bi Georgina Bundalla alimwakilisha Mkuu wa Mkoa huo kama mgeni rasmi.

Desmola Salo (37) aliliambia gazeti hili kuwa vyandarua vinavyotolewa na serikali havitoshi. “” mimi mwenyewe pale nyumbani ninayo familia ya watoto watano, lakini tunacho chandarua kimoja tu ambacho tunakitumia mimi na mume wangu huku watoto wakilala bila chandarua.”” Alilalamika Bi Desmola

Kwa upande wake Bi Evelina Haule (65) na Pendo Kayombo wao walikiri kupokea vyandarua vyenye dawa kutoka kwa mawakala wa mabadiliko katika jamii lakini wao wakaweka bayana kuwa wanatumia vyandarua hivyo kwa kujifunika nje ya shuka kama blanketi kwa kuwa hawajui matumizi vyandarua hivyo.

Bi Georgina Bundalla Mkuu wa Wilaya ya Ludewa aliwataka wananchi kuacha mara moja tabia ya kuamini na kuhusisha ushirikina na ugonjwa wa malaria kwa sababu wanapoteza muda na nguvu nyingi kwa waganga wa kienyeji wakati dalili za malaria ziko wazi ni vema kwenda Hospitalini kupima kwanza kuliko kukimbilia ushirikina. Aliongeza Bundala

“Tunasema malaria haikubaliki kwa sababu inawezekana kuidhibitiwa. Kwa nini ukubali kitu ambacho kinakuletea madhara. Malaria kwanza ina tabia ya kupunguza damu, wengi wetu tuna tabia ya kuchelewa kwenda hospitali na kuwahi kwa mganga wa jadi ambako tunachanjwa na kupunguzwa damu tabia hiyo ife,” alikemea

Meneja wa PSI Kileo Optatus alimwambia mgeni rasmi kuwa malaria ni ugonjwa hatari ambao unaongoza duniani kila baada ya dakika tano hufariki dunia ambapo katika bara la Afrika hasa nchi zilizo chini ya jangwa la Sahara na kuongeza kuwa Tanzania ni nchi ya katika Afrika kwa vifo vinavyotokana na malaria.

“wananchi wa Mbwila na Ludewa kwa ujumla tukishikiana na wadau wengine mbalimbali kwa kuzingatia kanuni zinazotolewa na wizara ya Afya kwa kutumia vyandarua vyenye dawa kila siku kwa mwaka mzima tutafanikiwa kuutokomeza ugonjwa huu wa malaria.”” Alisisitiza Bw Kileo

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Bw Happines Ndosi alimwambia mgeni rasmi kuwa ugonjwa huu ni hatari hasa katika makundi maalumu kama wajawazito na watoto waliopo chini ya miaka mitano na kwa Kitaifa maadhimisho haya yalifanyika mkoani Arusha kimkoa maadhisho haya yalifanyika wilayani Ludewa na kiwilaya yalifanyika kijiji cha Mbwila.

Mratibu wa malaria mkoa wa Iringa Bi Linda Chatila akitoa takwimu za ugonjwa wa malaria ailimwambia mgeni rasmi kuwa ugomjwa wa malaria unaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa wa nje yaani (OPD) na wale wanaolazwa katika mkoa.

Bi Linda alisema mwaka 2009 malaria iliongoza wagonjwa wa nje chini ya miaka mitano walikuwa asilimia 34.8 ya wagonjwa wote wa umri huo, pia kati ya wagonjwa wote waliolazwa umri chini ya miaka mitano malaria isiyokali iliongoza kwa asilimia 36.6 ya wagonjwa wote waliolazwa katika umri huu. Aidha ugonjwa wa malaria kali uliongoza kwa vifo kwa asilimia 19.5 ya vifo vyote vilivyotokea katika wagonjwa wa kulazwa wenye umri chi ya miaka mitano.

Alisema kwa wagonjwa wa nje wenye umri wa zaidi ya miaka mitano ugonjwa wa malaria ulichukua nafasi ya kwanza sawa na asilimia 24.8 ya wagonjwa wote wa umri huu takwimu hizi zinaonesha kuwa tatizo la malaria bado linaongezeka ingawa jitihada mbalimbali zimefanywa ili kudhibiti tatizo hili.

Wadau wengine wanao jishughulisha na mapambano dhidi ya malaria katika Nyanja mbalimbali mkoani wa Iringa ni pamoja na PSI (T), Chama cha Msalaba mwekundu, Meda, Tagurode, na maajenti wa kuleta mabadiliko katika jamii ambao shughuli zao ni pamoja na kusambaza vyandarua.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...