Skip to main content

TIMU YA PERAMIHO YAIBAMIZA TIMU YA SERIKALI 4-2, MEI MOSI

Na Friday Simbaya,


Peramiho

Timu ya wafanyakazi wa misioni ya Abasia Peramiho imeichapa Timu ya watumishi wa serikali mabao 4-2 Jumapili katika mashindano ya Mei Mosi 2011, yaliyofanyika katika viwanja vya Peramiho misioni, yakiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani, wilayani Songea vijijini mkoani Ruvuma.

Katika mechi hiyo kipindi cha kwanza timu zote mbili ziliaanza kwa kushambuliana, ambapo timu ya Peramiho Misioni walifanikwa kupata magoli mawili ya chapuchapu ambapo timu ya watumishi wa serikali hawakupata chochote hadi kipindi cha kwanza kimalizika.

Kipindi cha pili kilipoanza timu ya watumishi iliaamka kutoka usingizini na kushumbulia lango la abasia ya Peramiho bila mafanikio na matokeo yake kuaacha mwanya kwa timu ya Abasia kuongeza magoli mengine mawili.

Timu ya Abasia walibweteka na ushindi wa magoli manne na kuwadharau ndipo timu ya watumishi walicheza kufa na kupona na kurudisha magoli mawili dakika za mwisho na mpira kumaliza kwa matokeo 4-2, ambapo timu ya Abasia walitoka kifua mbele na zawadi ya shilingi 50,000/=.

Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Jenista Mhagama alikuwa nidiye mgeni rasmi na mfadhili wa mashindano hayo ya Mei Mosi 2011, alishukuru timu zote mbili kwa kujitokezana kucheza vizuri bila ugomvi.

Wageni wengine walioambatana na mbunge huyo ni pamoja na Diwani wa Peramiho Izack Mwimba, wenyeviti wa vijiji vya Peramiho ‘A’ na Peramiho ‘B’ na watendaji wa vijiji hivyo.

Mbunge huyo ambaye ndiye mfadhili wa mashindano yaliyoshirikisha timu za soka za wafanyakazi wa misioni na watumishi wa serikali na kukabidhi zawadi ya shilingi hamsini taslimu (50,000/=) kwa timu wa Abasia Peramiho na timu ya watumishi wa serikali nao waliambulia shilingi 30,000/=.

Kwa upande wa mchezo wa mpira wa pete timu ya Abasia iliibuka na ushindi wa mezani baada ya timu ya watumishi wa serikali kushindwa kufika kiwanjani, na kupatiwa zawadi ya shilingi 50,000/-.

Aidha, mbunge huyo wa Peramiho alielezea kupungua kwa zawadi kwa mwaka huu ikilinganishwa na mwaka jana kuelekeza nguvu kwa timu ya soka ya Wilaya ya Songea vijijini daraja la kwanza itakayo wakilisha mashindano ya ligi ya daraja.


Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Jenista Mhagama (katikati) akifantilia mashindano ya Mei Mosi kwa makini akiambatana na Diwani wa Peramiho, Izack Mwimba (wa kwamza kushoto)

Timu ya wafanyakazi wa Abasia ya Peramiho ya wanawake upande mpira wa pete.


Mbunge Jenista Mhagama akisalimia Timu ya watumishi wa serikali kabla mechi kuanza katika viwanja vya Peramiho.


Mpira wa kona katika lango la Timu ya Peramiho wenye jezi ya mistali mweupe na golikipa wao mwenye tracksuit ya rangi damu ya mzee.

Kiongozi wa Timu ya Abasia (Netiboli) akipekea zawadi kutoka kwa mbunge Jenista Mhgama wa pili kutoka kulia.

Timu ya watumishi wa serikali wakipata zawadi ya shilingi 30,000/= kama mshindi wa pili katika mchezo wa soka.


Mabingwa wa mashindina ya Mei Mosi 2011 ambao ni Timu ya Abasia ya Peramiho wa kupita zawadi ya 50,000/= kutoka kwa mbunge, ikiwakirishwa na kepteni timu mwenye t-shirt ya bendera ya Marekani na begi mgongoni.



Timu ya wafanyakazi wa Abasia Peramiho katika picha ya pamoja kwa mechi.





Timu ya soka ya watumishi wa umma katika picha ya pamoja kwa kabla ya mechi.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...