Skip to main content

WASOMALI 87 KIZIMBANI KWA KUINGIA NCHINI BILA KIBALI






WAKIMBIZI 87 wa kabila la wahadia kutoka nchini Ethiopia wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi wilayani Ludewa kwa kosa la kuingia nchini kwa makusudi bila ya kibali chochote huku wakijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Waethiopia hao ambao idadi yao kubwa ni wakristo na muislamu mmoja walikamatwa huko mwambao wa ziwa Nyasa katika kijiji cha Ngelenge Manda wakiwa wanajaribu kuvuka ziwa kwenda nchi jirani ya Malawi ambako wanakwenda kuomba hifadhi kutokana na kukimbia machafuko ya kisiasa nchini kwao.

Akisoma mashtaka mbele ya Hakimu mkazi wa mahakama ya Wilaya ya Ludewa Emanuel Mwambeta (DM) mwendesha mashtaka mratibu msaidizi wa polisi ambaye ni Mkuu wa upelelezi wilaya ya Ludewa ASP Thomas Mtikatika aliiambia mahakama hiyo kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo April 13 mwaka majira ya tano asubuhi huko Ngelenge Manda mwambao wa ziwa Nyasa.

Bw Mtikatika aliendelea kuiambia mahakama hiyo kuwa wakimbizi hao wamevunja sheria chini ya kifungu na 31 (1) (i) sheria namba 7 ya uhamiaji ya mwaka 1995 na kwamba kama watapatikana na hatia sheria itazingatiwa ikiwa ni pamoja na kurejeshwa nchini kwao.

Naye Bw Ali Abeid ambaye yuko kitengo cha sheria doria na uchunguzi katika idara ya uhamiaji wilayani Njombe aliongeza kuwa kwa mujibu wa sheria wanaweza kuhukumiwa chini ya kifungu na 31 au kwa mamlaka ya waziri anaweza kutumia kifungu na 14 kinampa mamlaka waziri kumrudisha mhamiaji haramu alikotoka.

Wao dhamira yao ni kwenda Afrika kusini kupitia Malawi na kwamba vipenyo vya kwenda nchi za kusini viko vitatu ambavyo ni Wilaya ya Kyela, Ludewa mkoa wa Iringa na Mbambabay mkoani Ruvuma maeneo hayo ndiyo yanayo sumbua. Hata hivyo washtakiwa wote walikiri kosa na sasa wanasubiri kurudishwa nchini kwao.

Alisema mikakati iliyopo ni kuzima mtandao wa mawakala wanaojihusisha na biashara hiyo ya kuwasafirisha wakimbizi hao haramu kwa manufaa binafsi, kesi hiyo imesikilizwa tena Mei 2 mwaka huu kwa kutekeleza amri kuridishwa kwao kwa mujibu wa mamlaka ya waziri wa mambo ya ndani ya nchi.

“”Awali wahamiaji haramu idadi yao ilikuwa 88, lakini mmoja alifariki dunia April 9 mwaka huu katika kundi la kwanza kutokana na kuugua malaria, kaharisha na kubadili hali ya hewa.”” Alisema Bw Alli

Katika kesi nyingine kijana Jackson Luoga (15) amehukumiwa kifungo kwenda jela mia miwili kwa kosa la kuiba kuku wenye thamani ya shilingi 45,000.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...