Skip to main content

VIBALI VYA MADINI LUDEWA

LUDEWA

WANANCHI Wilayan ya Ludewa mkoani Iringa wako hatarini kugeuka wakimbizi katika siku za usoni kutokana na hofu ya maeneo yao kugawiwa kinyemela na ofisi za madini kanda zilizoko mkoani Mbeya imefahamika.
Hofu na mashaka vilitanda hivi karibuni kwa madiwani wote walipotembelea katika Kata ya Iwela ambako kulikuwa na wasiwasi miongoni mwa wananchi waishio katika maeneo hayokuwa baadhi ya wachimbaji wageni wenye mitambo wasio na vibali wameingia na kuvamia kwa kuanza shughuli za uchimbaji bila wananchi kujulishwa.
Katika Baraza la Madiwani (Full Council) madiwani katika halmashauri hiyo waliitaka Wizara ya Nishati na Madini kutumia busara na uungwana kuhusu suala la ugawaji maeneo kwa sababu pamoja na kuwepo Sheria za Madini,  lakini wananchi nao wanayo haki ya kusikilizwa na kuhusishwa ili kuepusha migongano ya baadaye.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Bw. Matei Felician Kongo akizungumza katika baraza hilo alioneshwa kusikitishwa kwake kusikia kila eneo ndani ya wilaya  limetolewa kibali bila wananchi kujulishwa kwa kufanya hivyo usalama wa wanaLudewa huko wapi kama eneo lote limejaa vibali? Aliuliza Bw.  Kongo huku akimwagiza mkurugenzi kufuatilia.
Kwa upande wake Bi. Hilda Lauwo ambayo ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ludewa alisema ni hatari sana kama wananchi hawaelewi kama maeneo yao ya makazi yamegawiwa kinyemela na kwamba watakapokuja kujua na kutakiwa kuondoka itatuletea matatizo na hasara kubwa kwa sababu uzoefu umeonekana katika maeneo ya wenzetu.
Bi.  Lauwo alisema tumeona matukio mengi ya mauaji huko kwenye maeneo ya madini na kuongeza kuwa kuna haja ya kufuatilia jambo hili kwa wahusika ili kujua mstakabali wa wilaya, hatutaki yaje yatukute na sisi baadaye.
“Kama hatutapata ufumbuzi wa hili tatizo mapema tutakuja kupata shida kubwa baadaye, hivyo ni vema kamishna wa madini kanda aje atueleze na wananchi waelewe mapema kabisa kabla haya mambo hayajakuwa magumu,”alisisitiza Bi. Lauwo.
Aliongeza kuwa bila kufanya hivyo hii Wilaya ya Ludewa itakuja kuwa na matatizo kuliko wilaya zingine kwa hiyo ni vizuri wananchi wakaambiwa na kujulishwa maeneo yote yaliyokwisha kugawiwa na pengine kamishna aeleze ni vigezo gani alitumia kugawa maeneo yote ya Wilaya hii bila taarifa na inasemekana hadi sasa kuna vibali 70 vimeshatolewa.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...