Skip to main content

WANANCHI LUDEWA HAWAJUI HATIMA YAO

WAKATI Taifa linadhimisha miaka 50 ya Uhuru wananchi katika Kata za Mundundi na Mkomang’ombe ya Wilaya Ludewa, Mkoa wa Iringa ni zaidi ya miaka miwili sasa wamekaa tu bila kufanya shughuli za maendeleo kutokana na maeneo wanayoishi kuwa ndani ya migodi ya madini ya chuma na makaa ya mawe.


Aidha katika hali nyingine maeneo mengi ndani ya Wilaya ya Ludewa yanamilikiwa na watu wasiojulikana kwa kupewa vibali na ofisi ya madini kanda ya mbeya huku wenyeji wakibaki midomo wazi wasijue la kufanya.

Hayo yalibainishwa hivi karibuni na madiwani wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa walipofanya ziara ya kushtukiza katika Kata ya Iwela na kuwakuta wachimbaji waliodhaniwa kuwa ni wavamizi wakiwa na vibali kamili na ndipo walipofumbuka macho baada ya kuona ramani inayoonesha vibali zaidi ya 70 vilivyotolewa na kamishna wa madini kanda ya mbeya.

Ni kutokana na hali hiyo, madiwani katika Baraza kuu walimtaka kamishna wa madini kanda ya Mbeya kufika haraka Ludewa kwa ajili ya kutoa ufafanuzi juu ya ni vigezo gani alitumia kutoa vibali hivyo katika makazi ya watu bila kuwataarifu wenyewe.

Madiwani hao walionya kuwa kama hali itabaki kama ilivyo ni wazi siku za mbeleni Ludewa itakujakuwa na migogoro mikubwa kuliko sehemu yoyote ile nchini kutokana na wananchi hao kuonesha subira, utii na uvumilivu juu ya madini hayo tangu walipoambiwa na Rais wa Awamu ya kwanza Hayati Baba Mwalimu Julius Nyerere kuwa wasubiri.

Akipunguza jazba kwa madiwni hao Afisa tawala Wilaya ya Ludewa Bw. John Mahali alisema ofisi ya Mkuu wa Wilaya imeshafanya mawasiliano na kamishna wa kanda Mbeya na kuahidi kuja Ludewa kuendesha elimu kwa wananchi juu ya haki yao.

Pamoja na kumwita Kamishna wa madini bado wananchi wamepigwa na butwaa na sasa wanasubiri hatma yao kwa kutega masikio kwa kamishna wa madini kanda, ili kujua nini mstakabali wa maisha yao katika suala zima la madini ma makazi.





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...