Skip to main content

DC LUDEWA APUUZA MAAZIMO NA AGIZO LA BARAZA LA MADIWANI


 MKUU wa Wilaya ya Ludewa mkoani Iringa Bi. Georgina Bundala amepuuza maazimio na agizo la Baraza la Madiwani lililomtaka kuwakutanisha na Kamishna wa Madini Kanda ya Mbeya ili kujua sababu zinazopelekea wachimbaji na watafiti kuvamia maeneo mbalimbali ndani ya Wilaya hiyo bila wananchi kujulishwa na badala yake amemleta kamishna huyo kimyakimya na kuanza kumtembeza na kufanya mikutano ya hadhara kwa badhi ya Kata tu.

Katika Baraza Kuu la Madiwani (Fully Council) lililofanyika Ijumaa Julai 15 mwaka huu madiwani waliazimia na kuitaka ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi kumwandikia barua kamishina wa madini kanda ya Mbeya kufika Ludewa na kukutana kwanza na madiwani hao ili kujua nini kinaendelea wilayani mwao, sheria za madini zinasemaje kuhusu stahili na haki za mwananchi kwa watafiti na wachimbaji madini.

Katika Baraza hilo la madiwani Bi. Georgina Bundala alikuwa mgeni rasmi na baada ya kufungua baraza hilo aliondoka na kuwakilishwa na Afisa tawala wa Wilaya Bw. John Mahali na alitoa taarifa kuwa ofisi ya Mkuu wa Wilaya imewasiliana na madini kanda ili aje kutoa elimu kwa madiwani na baadaye kwa wananchi na baada ya elimu hiyo wananchi wataelewa haki zao.

Maazimio na maagizo ya madiwani hao yanatokana na madiwani hao chini ya mbunge wao kufanya ziara ya kushtukiza katika Kata ya Iwela ambako wananchi walilalamikia hatua ya watafiti na wachimbaji madini kuingia eneo hilo na mitambo bila taarifa jambo lililoleta usumbufu kwa wananchi.

Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda Bw. John Shija alisema Sheria na Kanuni za Madini ziko wazi, kwamba mtu anapopewa shughuli ya utafifiti au uchimbaji, lazima aende kwenye mamlaka husika, kwa Mkuu wa Wilaya ambaye humpeleka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri husika, naye kuwafikisha na kuwatambulisha mpaka ngazi ya kijiji au eneo husika ili kuondoa migongano.

Bw. Shija aliongeza kuwa baada ya mtafiti au mchimbaji huyo kufika katika Serikali ya Kijiji husika ndipo wanakaa pamoja na kuangalia na kuainisha ni lini shughuli za utafiti au uchimbaji zitaanza na hatimae kuwajulisha wananchi na mtu asiyepiga hodi kwa mwenyeji huyo ni mvamizi.

“Hao watu waliokuja kutafiti katika Kata ya Iwela walifika ofisi ya kanda tukawapa barua ya kuwatambulisha kwa Mkuu wa Wilaya ya Ludewa, sasa kilichoendelea huko sisi hatuhusiki kabisa kwa sababu hiyo ni mamlaka nyingine,” alisema Bw. Shija kwa msisitizo.
Bi. Monica Mchiro Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Wilaya ya Ludewa, ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Ludewa aliwaambia wananchi kuwa suala la kuingia watafiti na wachimbaji madini hata madiwani hawana taarifa ndiyo maana waliingia gharama na kwenda kujionea hali halisi kule Iwela. “Kama utaratibu huu ungefuatwa Halmashauri isingeingia gharama ya kuwasafirisha madiwani wote 34 na wabunge wawili kwenda eneo la tukio huu ni uzembe” alisikitika Monica.

Nao wananchi waliohudhuria mkutano huo wa hadhara katika viwanja vya stendi walisema tatizo siyo watafiti na wachimbaji tatizo liko kwa Mkuu wa Wilaya kuwakumbatia wawekezji hao kwa maslahi binafsi, kwanini hawakufuata utaratibu kama alivyoelekeza kamishna wa madini Bw. Shija ambaye ni muwazi.

“Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wao ni wapita njia tu wanafanya haya kwa maslahi yao binafsi ili baadaye tutakapokuwa tumeanza mvutano kati ya mwekezaji na wananchi wao watakuwa wameshahama” alilalamika Mzee Timothy Mtitu.

Hata hivyo pamoja na kamishna wa madini kanda kuanika utaratibu unaotakiwa kufuatwa Mkuu wa Wilaya aligeuka bubu na kushindwa kueleza lolote kuhusu alichokifanya kwa watafiti wa Kata ya Iwela, alichokumbuka ni kumfukuza mwandishi wa habari asipige picha mkutanoni hapo kana kwamba kulikuwa na usiri wowote.

“Mimi swali langu ni moja tu kwako Mkuu wa Wilaya naomba ujibu tujue wote kama kweli wewe unatenda kazi zako kwa haki, taratibu na sheria kwanini umemkataze mwandishi wa habari kufanyakazi yake katika mkutano huu wa hadhara,” aliuliza kwa jazba Bw. Amani Chaula.

Kwa mujibu wa kamishna wa madini maeneo mengi katika Wilaya ya Ludewa yamepewa vibali vya utafiti, lakini hadi sasa hakuna aliyeanza kuchimba na kuongeza kuwa kilichelewesha kuchimba makaa ya mawe ni kutokana na madini hayo kutegemeana, ndiyo maana serikali imeamua mwekezaji anayetaka makaa lazima awekeze pia katika chuma ili kwenda sambamba. 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...