Skip to main content

DIWANI LUDEWA AMKANA DC MKUTANONI, AGEUKA BUBU KUJIBU MASWALI LIKIWEMO LA KUMFUKUZA MWANDISHI WA HABARI




Na Friday Simbaya,
Ludewa
DIWANI wa Kata ya Ludewa ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludew, Bi Monica Mchiro juzi alimkana hadharani Mkuu wa Wilaya hiyo Bi Georgina Bundala kutokana na mkuu huyo kutokuweka bayana kilichotokea kati ya wananchi na watafiti wa madini walioingia na mitambo na kuanza shughuli katika Kata ya Iwela bila taarifa kwa madiwani na kuzua hofu na mkanganyiko kwa wananchi.
Bi Monica alifikia hatua hiyo ya kuwaambia wananchi ukweli baada ya Naibu Kamishna wa Madini Kanda ya Mbeya Bw. John Shija kuweka wazi Sheria za Madini na jinsi walivyotekeleza baada ya kutoa leseni ya utafiti katika kata ya Iwela na hatimaye wananchi kugundua kuwa tatizo lilikuwa katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi.
Bi. Monica pamoja na wapigakura wake walikuwa wametega masikio na kutegemea kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Bi Georgina Bundala angetoa ufafanuzi juu ya utata uliokuwepo kati ya wananchi na wachimbaji madini waliokuwa wameingia na mitambo katika kata hiyo na kuzua utata jambo lililopelekea madiwani wote pamoja na wabunge kufanya ziara ya kushtukiza na kuiingizia hasara halmashauri.
“Ndugu wananchi sisi madiwani wenu tulivyosikia mkanganyo kuhusu watafiti na wachimbaji hao walioko katika Kata ya Iwela tuliamua kufanya ziara ya kushtukiza, lakini tulikuta wahusika wana vibali vyote ikiwemo barua ya Mkuu wa Wilaya. Jambo hili lilituudhi sana kwani kama walikuwa wanajua kwanini wasituambie mpaka Halmashauri ikaingia gharama ya kuwasafirisha madiwani wote 35 bila sababu wangetuambia,” aling’aka Monica.
Awali, Bw. Shija aliwaambia wananchi kuwa baada ya watafiti hao kupewa leseni na kamishna wa Madini Kanda. “Tulimwandikia barua Mkuu wa Wilaya kuwatambulisha kwake ili utaratibu ufuatwe wa kuwafikisha hadi kwa walengwa kijijini.”
“Tukishatambulisha mtafiti au mchimbaji kwa Mkuu wa Wilaya husika siyo jukumu letu tena kufuatilia mamlaka nyingine, lakini sheria inasema kamishna akishatambulisha ugeni kwa Mkuu wa Wilaya ni jukumu lake kuwatambulisha kwa Mkurugenzi na yeye kuwapeleka na kuwatambulusha katika ngazi zote hadi ulipo mradi,”alibainisha Bw Shija.
Madiwani katika baraza kuu waliiomba ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Halmashauri kumwita kamishna wa madini kanda ili akutane na madiwani hao ili na wao waweze kujiridhisha na kuwaondolea utata uliokuwepo, lakini wakashangaa kamishna huyo akitembezwa na Mkuu wa Wilaya katika baadhi ya Kata wakati Ludewa yote imefunikwa na madini.
Baada ya kamishna kufafanua na kueleza kwa uwazi kuhusu utaratibu ulitumika ndipo maswali yakaanza. “Mimi swali langu ni moja tu kwako Mkuu wa Wilaya naomba ujibu tujue wote kama kweli wewe unatenda kazi zako kwa haki utaratibu na sheria kwanini umemkataze mwandishi wa habari kufanyakazi yake katika mkutano huu wa hadhara,” aliuliza kwa jazba Bw Amani Chaula.
Swali ambalo lilimtesa na kumnyima raha Mkuu huyo na kushindwa kujibu jambo lilizua mashaka kwa wananchi.
“Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wao ni wapita njia tu wanafanya haya kwa maslahi yao binafsi ili baadaye tutakapokuwa tumeanza mvutano kati ya mwekezaji na wananchi wao watakuwa wameshahama,”alilalamika mzee Timoth Mtitu.
Monica aliwaambia wananchi kuwa utaratibu alioueleza Kamishna ni mzuri, lakini sijui kwanini haukufuatwa na viongozi wetu wa Wilaya halafu mbaya zaidi wakauchuna bila kutushirikisha madiwani wote na wabunge.
Monica, “madiwani hawakujua kama watafiti na wachimba madini walioko Iwela walipita na kupata baraka zote kutoka katika ofisi za Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi tungejua tusingekwenda ilikuwa ni aibu tupu tulipofika tulioneshwa vibali vyote ikiwemo barua ya Mkuu,” alisikitika Monica.
Bi Monica alisema Julai 14 mwaka huu madiwani na wabunge wawili walifanya ziara ya kushtukiza katika Kata ya Iwela kutokana na hofu iliyokuwepo kuwa baadhi ya vigogo  wamehusika kuwaleta watafiti na wachimbaji hao kinyemela kwa manufaa yao binafsi.
Kwa mujibu wa ratiba baadhi ya kata alizopelekwa kamishna wa madini kanda ya Mbeya kutoa elimu kwa wananchi ni pamoja na Manda, Iwela, Mkomang’ombe, Lugarawa na Mundindi tu badala ya wilaya nzima.
Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...