Skip to main content

DKT MFUTAKAMBA: ZAIDI YA BILIONI 6 KUBORESHA USAFIRI WA MELI ZIWA NYASA,V ICTORIA NA TANGANYIKA



LUDEWA             
SERIKALI imetenga zaidi ya shilingi bilion 6 kwa ajili ya kuboresha usafiri wa Meli katika maziwa matatu nchini likiwemo Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa ambalo ni ziwa pekee lenye kero na changamoto kwa wananchi wa Ludewa, Songea na Mbeya.
Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt Athumani Mfutakamba alipotembelea Kata ya Masasi na Manda Wilayani Ludewa kujionea mwenyewe eneo kitakapojengwa kiwanja cha ndege katika kijiji cha Sagalu kama njia ya kuvutia wawekezaji kufika na kuwekeza Wilayani humo.
Dkt Mfutakamba alisema kuwa ujenzi wa uwanja wa ndege Sagalu Wilayani Ludewa utasaidia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi na kufungua milango ya kimaendeleo zaidi wilayani humo kutokana na kuwa na utajiri wa madini ya chuma na makaa ya mawe na dhahabu.
Hata hivyo waziri huyo aliahidi kuwa ujenzi wa uwanja huo muhimu utaanza mara baada ya wataalam wa viwanja vya ndege kufika na kulifanyia uchunguzi wa kina eneo hilo.
“Eneo nimeliona linafaa lakini kama serikali sasa tunaiachia jukumu hili Mamlaka ya viwanja vya ndege nchini ili kuangalia uwezekano wa kuufufua uwanja huu na kuuboresha sanjari na uwanja wa ndege Njombe kama njia ya kupanua wigo wa uchumi katika mikoa ya kusini.”” Alisema Mfutakamba.
Mfutakamba aliainisha kuwa fedha hizo kwa upande wa Ziwa Nyasa zitatumika kuboresha usafiri wa meli na kujenga magati na bandari katika mwambao wote wa Ziwa Nyasa ambako hadi sasa hakuna bandari ya uhakika.
Aliongeza kuwa wananchi wilayani Ludewa wanaendelea kuyalinda na kuyatazama madini kwa macho huku wenyewe wakikabiliana na umaskini wa kipato unaosababishwa kwa kiasi kikubwa na ukosefu wa miundombinu hafifu, kukosekana kwa viwanja vya ndege ndani ya wilaya hiyo ambapo utajiri ulioko umegeuka mateso kwa wananchi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wilayani humo wamesema miradi ya Mchuchuma na Liganga ni moja kati ya miradi mikubwa nchini lakini wakaishangaa serikali kusuasua kuanza utekelezaji.
Walisema kama miradi ya makaa ya mawe ya ketewaka, mchuchuma na chuma cha magangamatitu na Liganga itaanza vijana wengi watapata ajira pamoja na Taifa kuondokana na mgao wa umeme kwa sababu mradi huo peke yake unaweza kuzalisha megawati 600 hadi 1000.
Pamoja na mradi huo kuwapatia vijana ajira lakini pia utapunguza umaskini uliokithiri miongoni mwa wananchi kwa kutoa fursa mbalimbali kama sekta ya biashara kutokana na ongezeko kubwa la watu wanaotarajia kuja Ludewa kufanyakazi mgodini.
Eneo la Sagalu linalotarajiwa kujengwa uwanja wa ndege wilayani Ludewa awali katika miaka ya sabini liliwahi kutumika na Jeshi la Wananchi wa Tanzania ya Ulinzi na Usalama kipindi cha utawala wa Ngwazi Kamuzu Banda Rais wa kwanza wa Malawi, aliyejiita wa Muyaya alipojaribu kuchukua ardhi ya Tanzania upande wa Ziwa Nyasa na kusema ni eneo lake.
                             MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...