Skip to main content

UHABA WA MADAWATI LUGARAWA WANAFUNZI SABA WAKALIA DAWATI MOJA. FUNZA NI CHANGAMOTO KWA WATOTO HAO



   

Wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Lupefu, Lugarawa wakiwa darasani na Mwalimu Mary Mhagama huku wakiwa wamebanana saba kwenye dawati moja lenye uwezo wa watoto watatu.

WANAFUNZI katika Shule ya Msingi ya Lupefu iliyoko Kata ya Lugarawa wilayani Ludewa, mkoani Iringa wako hatarini kukatika miguu na viungo vingine vya mwili kutokana na kuliwa na funza mikono na miguu yao kunakosabishwa na uhaba wa madawati ambapo sasa wanafunzi saba wanalazimika kukalia dawati moja.
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bi. Aprudensia Lugome amekiri kuwepo kwa matatizo hayo na kuongeza kuwa hali hiyo inatokana na ukata wa fedha unaoikabili shule yake pamoja na uelewa na mwamko mdogo wa wananchi juu ya elimu.
Lugome alisema hulazimika kila wakati kununua pini madukani kwa fedha zake na kuwaita wazazi wa wanafunzi wenye mafunza kufika shuleni kushiriki kuwatoa funza watoto wao hata hivyo hufika wachache.
 Aidha aliongeza kuwa uchakavu wa majengo na ukosefu wa vitabu vya kujifunzia kunatokana nakusahaulika kwa shule ya Lupefu iliyoko upande wa kusini magharibi katika ya kata ya Lugarawa Ludewa.
Alisema kuwa shule hiyo ilianzishwa mwaka 1978 na kwamba hadi sasa ina jumla ya wanafunzi 545, madawati 149, vyumba 10 vya madarasa kati ya hivyo vyenye ubora vikiwa vitatu, walimu 15 lakini walio wengi wakiwa na matatizo ya kiafya.
Kuhusu utoro kwa wanafunzi mwalimu Lugome alimwambia mwandishi wetu kuwa watoto wengi wanatoka umbali mrefu wengine kilomita 6 hasa katika milima ya Luholomela na Msango na kwamba umbali huo husababisha wachoke na kuishia vichakani inakuwa vigumu kwa walimu na wazazi kugundua hali hiyo.
Kwa upande wa vyoo mkuu huyo alisema kuwa vyoo vyote vilivyopo ni vya muda tu na kwamba kwa sasa anajenga matundu 12 ya choo cha wanawake kutokana na fedha za faini kwa wazazi wa watoto wenye funza.
Alisema pamoja na hali hiyo watoto wamekuwa wakianguka hovyo na kupoteza fahamu shuleni hapo lakini cha kushangaza wakati mwingine huzinduka baada ya muda mfupi wakipelekwa hospitalini, hatimaye huendelea na shughuli kama kawaida.
Alizitaja baadhi ya changamoto zinazoikabili shule yake kuwa ni pamoja na ukosefu wa fedha za kuendeshea shule ambapo hulazimika kufanya vibarua kwa walimu na watu wengine sanjari na kuuza kuni na matete tunapohitaji kununua mahitaji ya shule.
Amewataka wazazi kuwekeza katika elimu na kufuatilia kwa karibu maendeleo ya watoto wao. Lakini akaishauri serikali kwenda na wakati kwa kutoa mafunzo kwa walimu hasa wanapobadili sera mpya ya elimu.
Serikali haijatoa mwongozo mpya namna ya kuendesha shule hasa baada ya MEM kuonekana inalegalega kwa kutopatikana kwa fedha mashuleni na sasa shule nyingi zinaendeshwa kwa kusuasua.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...