Skip to main content

VIONGOZI WA DINI MBALIMBALI LUDEWA WAPATA MAFUNZO JUU YA AFYA YA UZAZI NA MTOTO

Ludewa


ZAIDI YA VIONGOZI 53 wa dini mbalimbali wanawake kwa wanaume kutoka katika maeneo mbalimbali wilayani Ludewa, Mkoa Iringa wamehudhuria mafunzo ya siku tatu kuhusu Afya ya uzazi na mtoto.
Shirika lisilokuwa la kiserikali la IMA WORLD HEATH la jijini Dar es Salaam limetoa mafunzo hayo maalum kupitia mradi wa Maisha Program uliofadhiliwa na shirika la maendeleo la kimataifa la watu wa marekani USAID.
Awali akitoa taarifa kwa mgeni rasmi Mratibu wa mradi huo  Bw Joel Lubebe alieleza kuwa sababu ya kuwapa elimu hii viongozi wa dini mbalimbali ni kutokana na viongozi hao kuaminiwa na jamii, pia jamii kuwa tayari kupokea maagizo na mafundisho yao sanjari na ushawishi na vipawa walivyopewa na Mungu mwenyewe.
Bw Lubebe alisema mradi wa Maisha Program unalenga kupunguza vifo vya uzazi vinavyotokana na sababu za moja kwa moja kama kutokwa damu kupita kiasi kwa wajawazito baada ya kujifungua pia kupunguza vifo vya watoto wachanga na kupunguza kiwango cha watoto waliozaliwa na uzito pungufu kwa kuhakikisha akina mama wanatibiwa Malaria mapema.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Bi Hilda Lauo katika hotuba yake kwa washiriki wa mafunzo hayo alisema Tanzania imeandaa mpango mkakati wa kitaifa wa kuongeza kasi ya kupunguza vifo vya uzazi na mtoto kufikia robo tatu ¾ na 2/3 kwa vifo vya watoto ifikapo 2015.
Bi Lauo aliongeza kuwa mkakati huu unatoa fursa kwa wadau wote katika miradi yote kusisitiza katika maeneo mawili, utoaji wa huduma katika vituo, na huduma ya Afya ya jamii ili kufikia malengo ya mpango wa Taifa wa kupunguza umaskini na kuongeza uchumi Tanzania (MKUKUTA) na mpango wa Maendeleo wa Afya ya Msingi( MAAM).
Kwa upande wake Bi Velonica Mkusa mwezeshaji kutoka Ima World Heath alisema mradi umelenga kuwafundisha viongozi wa dini ili watumie miongozo yao kuhusu afya ya uzazi na mtoto katika kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii.
Mkusa alisema tatizo la vifo vitokanavyo na uzazi kwa akina mama na watoto ni kubwa kwani kati ya akina mama 100,000 watakaojifungua watoto hai 454 wanafariki dunia sababu ya uzazi na kuongeza kuwa kuna umuhimu kwa akina mama kuwahi cliniki mapema anapohisi ujauzito kwani husaidia kupata msaada mapema.
Naye Mratibu wa hudum za Afya ya uzazi na mtoto wilayani Ludewa Bi Imelda Mtemi (Mama Mnyagala) akitoa takwimu ya Wilaya yake alisema mwaka 2008 akina mama 139 walifariki dunia kutokana na vizazi hai 100,000 ambapo mwaka 2009 akina mama 85 walifariki na  2010 akina mama 108 walifariki dunia kutokana na vizazi hai 100,000.
Bi Mnyagala Mtemi aliongeza kuwa vifo vya watoto chini ya mwaka mmoja (IMR) mwaka 2008 vifo 26 vilitokea ambapo mwaka 2009 ilikuwa 25/1000 na mwaka 2010 vifo 25 kwa 1000 vilitokea.
Aliongeza kuwa akina mama waliojifungua katika vituo vya kutolea huduma za afya kwa mwaka 2008 ilikuwa asilimia 67 ambapo 2009 ilifikia asilimia 68 na mwaka 2010 ilifikia asilimia 69 na akina mama wanaojiunga na cliniki kabla ya miezi minne ya ujuzito mwaka 2008 ilifikia asilimia 68 ambapo mwaka 2009 ilishuka na kufikia asilimia 58 na mwaka jana ilifikia asilimia 59.
Hata hivyo, Mtemi alisema anakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo uelewa mdogo wa jamii katika kufanya maamuzi ya haraka juu ya kuwawahisha hospitali akina mama wenye matatizo ya uzazi, uelewa mdogo juu ya akujiunga na cliniki kabla ya miezi minne, juu ya lishe kwa wajawazito na muda wa kupumzika sanjari na kutumia dawa za Malaria kwa mjamzito
Akifunga mafunzo hayo Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Dr. Happenes Ndosi aliwashukuru wawezeshaji kutoka shirika la Ima World Heath kwa mafunzo hayo na kuwataka washiriki hao viongozi wa dini mbalimbali kufikisha elimu waliyoipata kwa waumini wao ili kupunguza vifo vya uzazi na mtoto wilayani mwake.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...