Skip to main content

WAFANYABIASHARA SOKO KUU LUDEWA WAMETELEKEZWA VYOO VICHAFU, HAVINA MAJI SOKO HALINA ULINZI.

Wengi sasa wafanyia biashara mtaani na majumbani.
WAKATI Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ikilalamikia ufinyu wa Bajeti na kushindwa kutekeleza miradi ya maendeleo na huduma muhimu za jamii kwa kukosa raslimali fedha, wafanyabiashara katika soko kuu la mjini hapa wamelikimbia soko na kuamua kufanyia majumbani bila kulipa ushuru kutokana na soko hilo kukosa huduma muhimu za kiutu kama vile choo safi, maji na mlinzi.
Wakizungumza katika soko jipya wafanyabiashara wa mbogamboga, nyanya, vitunguu na matunda walisema wanalazimika kukimbilia majumbani kwao hata kama ni mbali kwa ajili ya kwenda kujisaidia kutoka na soko hilo kuwa na vyoo vichafu vya zamani huku soko jipya nalo likikosa maji wakati vyoo ni vya kuflashi.
”Ndugu mwandishi hebu angalia na uingie wewe mwenyewe ndani ya vyoo hivyo kama unaweza kujisaidia na kuvumilia hali ya uchafu kila siku tunalazimika kwenda majumbani kujisaidia na kisha kurudi kuendelea na biashara.ni hatari sana inasikitisha,” alisema mmoja wa wafanyabiashara kwa masharti ya kutotajwa jina kuhofu kufuatiliwa.
Kwa upande wake Bi Jovita Haule na Neema Haule walisema ni kutokana na adha zilizopo katika soko hilo sasa hivi wafanyabiashara wengi wameondoka na kwenda kufanyia biashara majumbani na kuwafuata wateja waliko mitaani ambako kulipa ushuru ni nadra tofauti na sokoni ambako wanatozwa ushuru hata kama hawajauza.
Bi Auleria Mtitu (mama Grady) aliulaumu uongozi wa kiji na Kata wao ndiyo chanzo cha kuikosesha Halmashauri mapato kwa sababu wameshindwa kulisimamia soko kukidhi haja na kuruhusu watu kufanya biashara mitaani na majumbani ambako siyo rahisi kufuatilia ushuru ukuzingatia kwa sasa wengi wanalima mboga.
Mama Grady na wenzake walisema kuwa hakuna haja ya kulima mboga kama hali itaendelea kuwa kama ilivyo na kuongeza kuwa wakati umefika sasa wa viongozi wenye mamlaka kuwakusanya wafanyabiashara walioko mitaani na majumbani kuja sokoni ili kuleta ushindani wa kweli.””sisi tunalipa ushuru kila siku lakini wenzetu hawalipi mitaani hakuna usawa angalia mwandishi soko liko wazi halina watu kabisa walilalamika wafanyabiashara hao””.
Afisa Mtendaji Kata ya Ludewa Bw Onesmo Haule kwa upande wake alikiri kuwepo kwa wafanyabiashara kuzagaa mitaani na kusema kuwa watu wote wanatakiwa kuleta bidhaa zao sokoni, lakini akajitetea kuwa soko limejaa hakuna nafasi jambo ambalo lilipingwa vikali na wachuuzi hao kwa sababu soko liko wazi sasa limejaa watu wasioonekana? Waliuliza wachuuzi hao
Kuhusu ulinzi wa soko Bw Haule alisema hilo siyo jukumu la Halmashauri bali ni wajibu wa wafanyabiashara wenyewe kutafuta mlinzi wa kulinda mali zao na kwamba utaratibu huo walishakubaliana katika vikao vilivyopita chini ya uongozi wa soko hilo.
Mwenyekiti wa wafanyabiashara sokoni hapo mzee Masopola kwa upande wake alisema kwa upande wa vyoo hiyo ni hadithi ya muda mrefu sana na viongozi wamekuwa wakiahidi kila wanapoomba kura lakini hakuna kinachoendelea na wala hawatembelei kuona hali ilivyo.
Masopola alisema vyoo vilivyopo vimechoka mpaka vimechakaa na sasa vimezungushwa na mabati machakavu na kuongeza viongozi wamalazimisha watu kuingia katika soko jipya lakini huduma za msingi kama maji, vyoo na mlinzi hakuna hivyo watu wanalazimika kujitwisha mizigo kila siku kuleta sokoni na kurudisha na kushauri kuwa kama kuleta maji ni vigumu ni bora vichimbwe vyoo vya shimo.
”Mapungufu yapo pande zote kwa serikali na kwa wafanyabiashara hivyo kuna haja ya kukaa pamoja kuwaelimisha watu wajibu na haki zao lakini kwa upandewa serikali ijue wajibu zake na kuziweka bayana ama sivyo soko litabaki wazi kwa sababu mapungufu haya yalianza wakati wa kulikabidhi soko jipya hapakuwa na maandaliza wala utaratibu,”alisisitiza mzee masopola
                               

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...