Skip to main content

WALIMU WA VYUO VYA UFUNDI STADI WAPIGWA MSASA KUHUSIANA NA CBET

Walimu zaidi ya 30 wa vyuo mbalimbali vya ufundi kutoka katika mikoa ya nyanda za juu (Iringa na Ruvuma) wamefanya semina ya mafunzo yaliyodumu kwa takribani wiki mbili kwa lengo la kujengewa uwezo wa namna ya kutumia mfumo mpya wa kufundishia ujulikanao kama ‘Competence Based Education and Training’ (CBET).


Akizungumza na gazeti la Mwenge, Mratibu wa vyuo vya ufundi stadi vya VETA wa nyanda za juu Bw. John Mwanja amesema mafunzo hayo yamelenga kuwawezesha walimu wa vyuo vya ufundi stadi kutumia mfumo mpya wa kufundishia yani CBET.

Mfumo huo mpya wa kufundishia (Competence Based Education and Training (CBET) unatafsiriwa kuwa ni umiliki na uendelezaji wa ustadi, ufahamu, mitazamo sahihi pamoja na uzoefu ili kujiletea mafanikio katika utendaji wa majukumu ya kimaisha.

Bw. Mwanja amesema, endapo mfumo huu mpya utatekelezwa kama ilivyokusudiwa, basi utaleta mafanikio chanya zaidi ukilinganishwa na ule mfumo uliokuwa ukitumika hapo awali kutokana na ukweli kwamba mfumo huu mpya utawawezesha wanafunzi kuendelea kutoka katika hatua moja kwenda hatua nyingine.

“Katika mafunzo ya ufundi stadi tunachukulia ustadi kama nyenzo muhimu ambayo inajumuisha elimu, uelewa, ujuzi, utendaji, mtazamo pamoja na uzoefu,” alisema Mwanja.

“Mfumo mpya wa kufundishia ni maendeleo mapya kabisa ambayo yatawapa mwanya wanafunzi wa vyuo vya ufundi kuweza kuendelea kutoka hatua moja kwenda nyingine. Hii ina maana kuwa baada ya kupata cheti cha Daraja la tatu, mwanafunzi anaweza kuendelea na ngazi ya Diploma katika chuo chochote ambacho kinatumia mfumo mpya,” aliongeza Mwanja.

Hii ni semina ya pili kufanyika katika nyanda za juu wakati semina ya kwanza ilifanyika katika wilaya ya Njombe mkoani Iringa, ambapo ilihudhuriwa na walimu wa vyuo vya ufundi wapatao hamsini na tatu 53.

Haya ni marekebisho mapya ambayo yamefanywa na VETA kwa lengo la kuboresha viwango na sifa za ufundishaji katika vyuo vya ufundi ili kukidhi ushindani uliopo katika soko la ajira.

Bw. Mwanja pia amewaasa watanzania kuwa na ustadi wa kutosha ili waweze kupambana na changamoto za ushindani uliopo katika soko la ajira.

Kila jambo lenye mafanikio halikosi pia kuwa na mapungufu, ndivyo ilivyo pia kwa huu mfumo mpya wa CBET. Mapungufu hayo yameelezwa kuwa ni uhaba wa walimu wenye viwango na sifa zinazohitajika ili kumudu mfumo mpya pamoja na ukosefu wa vitabu.

Vile vile, kwa upande wa wanafunzi wanalazimika kusoma vitabu vingi vya masomo ya ziada ambayo hayakuwepo kwenye mfumo wa awali.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...