Skip to main content

KESI YA PEMBEJEO KATI YA AFISA MTENDAJI NA KATIBU WA CCM LUGARAWA YAAHIRISHWA TENA


Ludewa

KESI ya wizi wa mbolea ya pembejeo yenye thamani ya zaidi ya milioni sita inayowakabili Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Mdilidili Bw Otmari Kayombo Komnfoti, Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Lugarawa Bw Yohanes Mhagama Muafaka na wenzake imeahirishwa tena.
Akiahirisha kesi hiyo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ludewa Emanuel Mwambeta, Mwendesha Mashtaka Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Mtikamtika alimwambia hakimu kuwa mshtakiwa namba moja ametoa taairifa ya kuumwa.
Bw. Mtikamtika alikuwa amefika na mashahidi watatu akiwemo Askari Polisi Kitengo cha Upelelezi Bw. Kelvin Kapinga, Afisa kutoka Ofisi ya TAKUKURU Bw. Lucas Swebe na mkazi mmoja wa kijiji cha Mdilidili kwa jina la  Bonifasi Mlowe.
Katika kesi hiyo yumo pia wakala wa mbolea katika kijiji hicho Bw. Anazet Mlelwa na mwenyekiti wa pembejeo wa kijiji hicho Bi. Grace Komba ambao wote walikuwepo mahakamani hapo.
Kesi hiyo imekuwa na mvuto wa pekee kuliko kesi zingine mahakamani hapo kutokana na wananchi wengi kuguswa, kuchoshwa na unyanyasaji wanaopata kutoka kwa viongozi wa vijiji na mawakala kuhusu mbolea ya ruzuku katika maeneo yao.
Katika hati ya mashtaka washtakiwa walitenda kosa hilo Januari 5 mwaka huu majira ya saa kumi za jioni na kwamba kwa udanganyifu walikula njama na kuiba jumla ya shilingi 6,966,000/- kwa njia ya kugushi kwa kuandika majina hewa wakiwemo waliokufa, wagonjwa na watoto wadogo.
Washtakiwa wanakabiliwa na makosa mia tatu kulingana na idadi ya wananchi waliokosa na kutapeliwa mbolea katika kijiji cha Mdilidili katika Kata ya Lugarawa.
Katika kesi hiyo kosa la kwanza linaloangukia katika kifungu cha 306 linawakabili washtakiwa wote wanne ambapo kosa la pili la kugushi linawakabili Bw. Komnfoti mtendaji wa kijiji na Bi Komba chini ya vifungu vya 333,335(a) na 337 sura ya 16 inayosema Januari 5 mwaka huu washtakiwa waligushi vocha 300 za mbolea ya ruzuku.
Kesi hiyo yenye jumla ya mashahidi sita wa upande wa mashtaka imeahirishwa hadi Octoba 12 mwaka huu ambapo itakuja kwa kusikilizwa na hakimu kuagiza washtakiwa wote kuhudhuria siku hiyo bila kukosa.
Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...