Skip to main content

NYAMA YA NG’OMBE NA NGURUWE BEI JUU LUDEWA

















Ludewa


KUPANDA kiholela kwa bei za bidhaa mbalimbali wilayani Ludewa kunatokana na idara kadhaa ndani ya Halmashauri ya wilaya hiyo kutofanyakazi kwa ufanisi sanjari na ushirikiano hafifu uliopo kati ya idara na idara. 

Hayo yamethibitika kufuatia wafanyabiashara ya nyama ya ng’ombe na nguruwe mjini hapa kupandisha bei ya bidhaa hiyo kiholela huku mamlaka zinazohusika zikifumbia macho suala hilo kwa madai kuwa hazina taarifa na wakati mwingine kutupiana mpira juu ya nani awajibike.
Kwa mujibu wa wananchi na watumiaji wa bidhaa hiyo muhimu waliokutwa katika mabucha yaliyoko mjini hapa jana, walisema kilo moja ya nyama ya ng’ombe mchanganyiko imefikia shilingi 5,000 badala ya 4,000 ambapo steki ni shilingi 6,000 badala ya shilingi 5,000 na kwamba bei hizo zimeanza August 3 mwaka huu.
Kwa upande wake Afisa Biashara wilayani Ludewa Bi Martha Mfugale alipotakiwa kueleza ni kwanini bei imepande ghafla na kwa kiwango kikubwa alisema yeye mara ya mwisho alinunua nyama siku ya Sikukuu ya Eid el Fitr  kwa bei ya shilingi elfu nne.
Hata hivyo alisema kama ni kweli, kiwango kilichopandishwa ni kikubwa mno na kwamba hajui wachinjaji hao wametumia vigezo gani kufikia bei hiyo, lakini aliahidi kufuatilia suala hilo. Wafanyabiashara za chakula wamelalamikia bei hizo na kusema kuwa inawezekana hakuna serikali ndiyo maana watu wanaweza kuamuka asubuhi na kujipangia bei huku wananchi wenye kipato kidogo wasio na jukwaa la kusemea wakiendelea kuumia.
Afisa Mifugo Wilaya ya Ludewa  Bw Marco Mhagama yeye amekilaani kitendo kilichofanywa na wafanyabiashara hao wa nyama na kusema kuna haja ya idara ya biashara na idara ya mifugo kufanya kazi kama timu kwa kufanya ukaguzi wa mara kwa mara. Akifafanua kuhusu tozo na ushuru kwa wachinja nyama hao Bw Mhagama alisema kwa sasa ushuru wa Halmashauri ni shilingi elfu nne na mia tano kwa mchanganuo kuwa ushuru wa machinjio ni 2,000,ada ya mkaguzi yaani mtaalam ni shilingi 2,500 na serikali kuu shilingi 1,000.
Kwa upande wa nyama ya nguruwe Bw Mhagama alisema wao hawapaswi kupandisha bei kwa sababu ushuru huo hauwagusi wao kwa kuwa hawana machinjio maalum na kwamba hawarusiwi kutoa nguruwe nje ya kijiji kwa hiyo hakuna gharama.
Wakitoa mapendekezo yao wananchi wameitaka serikali kutoa bei elekezi kwa wachinjaji hao lakini wakawalaumu maafisa biashara na wale wa mifugo kuacha kung’ang’ania kukaa maofisini na kusubiri mishahara badala yake wafanye ukaguzi wa mara kwa mara siyo kwa wachinjaji tu bali na katika bidhaa zingine.
Wafanyabiashara hao wa mjini Ludewa wamejipandishia bei kiholela huku wakilaumiwa na wateja wao kwa kuchakachua mizani inayotumika katika mabucha, huku wakitumia mikokoteni kusafirishia nyama toka machinjoni. 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...