Skip to main content

DC LUDEWA, SITAYUMBISHWA NA WAWEKEZAJI WATAKAOVUNJA SHERIA ZA NCHI MCHUCHUMA NA LIGANGA.

Ludewa

MKUU wa Wilaya ya Ludewa mkoani Iringa Bi Georgina Bundala amekana kutoyumbishwa kwa namna yoyote ile na wawekezaji wataovunja sheria za nchi na zile zilizopo katika mikataba ya sheria ya madini ya Liganga na Mchuchuma.
Bi Georgina aliwaambia waandishi wa habari jana ofisini kwake ambao pamoja na mambo mengine walitaka kujua amejipanga vipi na nini msimamo wake kwa wawekezaji wenye tabia ya kuwayumbisha viongozi, hasa wakuu wa wilaya nchini waliopo ndani ya migodi kwa manufaa yao binafsi.
Aliongeza kuwa wawekezaji wengi nchini wanapokuja kuomba kuwekeza wanakuwa na nidhamu na kuonesha ushirikiano wenye kuleta ufanisi kwa nia nzuri ya kuchochea chachu ya kuwaletea maendeleo wananchi waishio maeneo ya migodi, lakini baadaye hugeuka na kuwafanya wananchi kuwa wakimbizi nchini mwao siko tayari kuwaonea aibu, alisisitiza.
“Sheria za nchi zipo wala sina haja ya kuumiza kichwa na kupoteza muda mtu yeyote atakayekiuka au kuvunja sheria kwa lengo la kuwanyanyasa wananchi tofauti na makubaliano yaliyomo ndani ya mkataba wake na serikali kwa niaba ya wananchi sheria itafuata mkondo wake,” alisisitiza Bundala.
Aidha, mkuu huyo amewataka wananchi wilayani humo kuongeza kasi ya kuwapeleka na kuwapatia vijana elimu ya kutosha hasa katika Nyanja ya ufundi stadi kwa nia ya kuliteka soko la ajira pindi madini hayo yatakapoanza kuchimbwa kufuatia serikali kutiliana na wawekezaji wa ndani na nje baada ya kushinda zabuni.
Kuhusu Chuo cha Ufundi VETA kilichotakiwa kujengwa katika maeneo ya kijiji cha Shaurimoyo Kata ya Lugarawa, Bi Georgina alisema kuna uwezekano mkubwa wa chuo hicho kujengwa katika Kata ya Ludewa Makao Makuu ya Wilaya ya Ludewa kutokana na sababu kuu nne.
Alizitaja baadhi ya sababu zitakazofanya chuo hicho kujengwa mjini kuwa ni pamoja na chuo hicho kuwa karibu na huduma muhimu kama vile benki, ili kuwa na urahisi wa kupata fedha, hospitali, mawasiliano, usalama na kuwa jirani na ofisi za utawala.
Kutokana na hali hiyo madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa wanatakiwa kukaa upya ili kubadili mihutasari na kupeleka kwenye kikao cha ushauri cha wilaya (DCC ) tayari kwa kupeleka mapendekezo kwenye kamati ya ushauri ya Mkoa (RCC) kwa hatua.
Hata hivyo mkuu huyo wa wilaya aliwataka wananchi kuanza kujiandaa kwa kuchangamkia fursa zitakazotokana na uwekezaji kama vile matunda, mbogamboga, kujenga nyumba za kupangisha wageni wanaotarajia kuja wilayani Ludewa kwa shughuli mbalimbali.
Wataalamu na watafiti mbalimbali wa madini nchini wamegundua kuwa karibu ardhi yote ndani ya Wilaya ya Ludewa imegubikwa na madini kwa hiyo wananchi wasipojiandaa vema kuna hatari ya wao kuendelea kuwa maskini wa kipato huku wakiwaacha wageni wakinufaika na rasilimali hiyo.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...