Skip to main content

KIKWETE AKATA MZIZI WA FITINA KUHUSU GARI LA WAGONJWA MLANGALI AWALI WANANCHI WALIJIPANGA BARABARANI KUKUMBUSHA AHADI YA RAIS, MADIWANI WAPIGWA MSHANGAO

Ludewa

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete jana alikata mzizi wa fitina kutokana na utata uliokuwepo kati ya wananchi na Baraza la Madiwani kuhusu gari la wagonjwa  Namba SM 9192 aliloahidi kwa Kituo cha Afya Mlangali mwaka 2008.
Dr. Kikwete alifikia hatua hiyo baada ya wananchi wa Kata ya Mlangali waliokuwa wamesimama barabarani kumlaki na alipowataka watoe shida zao wakamwambia kuwa wanashukuru kwa kutimiza ahadi ingawa wameipata jana wakati gari hilo lina zaidi ya miezi saba wilayani.
Wananchi wa Mlangali pamoja na mambo mengine walimwambia Rais kuwa katika Kata yao wanakabiliwa na mambo mengi ikiwemo maji safi, barabara, gari la kubebea wagonjwa (Ambulance) na umeme.
Madiwani katika kikao chao cha Julai 15 mwaka huu walikubaliana kwa kauli moja kuchukua gari la kubebea wagonjwa (Ambullance) No. SM 4677 lililokuwa katika Hospitali ya Wilaya na kulipeleka Lupingu ili kuwahudumia wananchi wa Mwambao na gari SM 9192 lililotolewa na Rais kubakizwa wilayani huku, mbunge akiahidi kupeleka haraka gari jingine Mlangali.
Kutokana na utata huo wananchi wa Mlangali waliposikia ziara ya Rais waliamua kujipanga barabarani ili kudai haki yao kama alivyoowaahidi mwaka 2008 na siku moja kabla ya rais kufika walikabidhiwa gari kwa maandishi.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Matei Kongo kwa upande wake alisema kuwa gari SM 9192 lililetwa bila maelekezo ndiyo maana Baraza la Madiwani lililofanyika Julai 15 mwaka huu liliamua kwa kuzingatia vipaumbele na jiografia ya wilaya, lakini maelekezo ya rais ni sahihi tu aliongeza.
Katika barua yake kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, Katibu Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ilielekeza kuwa gari lenye namba za usajiri SM 9192 lililokabidhiwa Aprili 01 mwaka huu ni kwa ajili ya kutekeleza ahadi ya Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano na lilitolewa kwa ajili ya matumizi ya Kituo cha Afya cha Mlangali.
Diwani wa Kata ya Mlangali Bw. Rudolf Kacheche Chaula kwa upande wake alisema rais alitoa ahadi hiyo mwaka 2008 na gari hilo kufika wilayani Ludewa mwezi April mwaka huu, lakini limekabidhiwa Mlangali Novemba 11 mwaka huu takribani miezi saba limekaa nje.
Kacheche alisema yeye na wananchi wake wanamshukuru rais kwa maamuzi hayo, na kwamba hakuna sababu ya kutafuta mchawi kwa sababu aliyetoa ndiye aliye elekeza matumizi ya gari hilo ingawa hakuzuia gari hilo kutumika mahali popote ndani na nje ya Halmashauri.
Aliongeza kuwa baraza la madiwani lililokaa na kuelekeza gari la wagonjwa namba SM 9192 libaki katika Hospitali ya Wilaya na SM 4677 lipelekwe Lupingu lilizingatia jiografia ya wilaya na kwamba nia ilikuwa nzuri tu, lakini kwa kuwa aliyeleta ndiye aliyeelekeza vinginevyo inabidi tukubali.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...