Skip to main content

LHRC, YAAMSHA MADIWANI LUDEWA, NI KUHUSU HAKI ZA BINADAMU NA WAJIBU ZAO.

Ludewa
 
HUKU Tanzania ikiadhimisha miaka Hamsini ya Uhuru madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa katika Mkoa Iringa bado wanabanwa na mfumo wa utawala na kushindwa kusimamia mali za umma.
Wakizungumza jana katika semina ya siku tatu kuhusu sheria za kazi, rushwa na utawala bora, haki za binadamu, Katiba, wajibu na maadili ya diwani, iliyoendeshwa na Kituo Cha Sheria na Haki za Binadamu walipongeza kituo hicho kwa kuwafumbua macho.
Madiwani hao walilalamikia mifumo na miongozo mibaya ya TAMISEMI inayoleta urasimu kwa nia ya kudhoofisha nafasi na hadhi ya madiwani kwa wananchi jambo linalopelekea kudharauliwa na watumishi wa Halmashauri.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Bw. Emanuel Mlelwa ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mafunzo hayo alisema mafunzo haya yamekuja wakati mwafaka kwa madiwani hao kutokana na wengi wao kutokujua vyema sheria, maadili na wajibu zao.
Mlelwa aliwataka madiwani kuwa wasikivu kwani mafunzo hayo ni ukombozi kwao kwa kuwa semina elekezi walizopewa hazitoshi kuwa kitendea kazi kwao kwa sababu hazifafanui vyema mambo ya sheria.
Akimkaribisha mgeni rasmi Bi Edina Lushaka ambaye ni mwanasheria kutoka kituo cha sheria na haki za binadamu cha jijini Dar es Salaam alisema nia ya kutoa mafunzo haya ni kuwapa madiwani elimu kuhusu haki za binadamu katika maeneo yao.
Lushaka alimwambia mgeni rasmi kuwa madiwani wanapashwa kujua wajibu zao na maadili ikiwemo kudumisha uhusiano baina yao na watumishi wa Halmashauri kama kanuni ya 25 hadi 28 inavyobainisha.
“Diwani kama kiongozi ni mtoa maamuzi, msimamizi, mwajiri na mdhibiti wa shughuli za Halmashauri na kwamba siyo mtendaji, bali ni mwakilishi anayewajibika kwa wananchi wake,” aliongeza Bi. Edina Lushaka.
Naye Bahati Mwanu katika mada zake aliwaeleza madiwani maana ya Katiba na historia ya katiba ulimwenguni, historia ya katiba Tanzania, historia ya haki za binadamu, vizazi na sifa za haki za binadamu utetezi, ulinzi wa haki na faida za kuheshimu haki.
Bi. Manu aliwataka madiwani kujua misingi, taswira na malengo ya kanuni za maadili yao, sifa binafsi za diwani, tabia ya hadharani ya diwani, mali, mapato, madaraka kisiasa ikiwemo uwajibikaji, maslahi na kinga na rufaa kwa anayeona ameonewa.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Bw Matei Kongo akiungwa mkono na madiwani wake, alisema Serikali kupitia TAMISEMI imekuwa ikiwabana na kuwapa watumishi nafasi bila kuwa na sifa.
Kongo alisema watumishi wengi wamekuwa wakikaidi maelekezo ya madiwani kwa majigambo na kujivunia TAMISEMI na kwamba diwani hana mamlaka ya kuwafukuza kazi na kuongeza kuwa hili ni tatizo linalosababishwa na mifumo mibaya serikalini.
Diwani ni kiungo kati ya Halmashauri na vijiji na mitaa na mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya Kata na anapashwa kujua hali ya uchumi inayowakabili wananchi anaowaongoza, uboreshaji wa huduma na shughuli za maendeleo zinazoweza kuwakwamua katika dimbwi la umaskini.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...