Skip to main content

MASHINDANO YA MGOSI CUP 2012

PASCAL MGOSI MDHAMINI


TIMU YA RED STARS WAKISHANGILIA GOLI

MASHABIKI WA TIMU YA RUWAWAZI AKIMURUSHA JUU KIPA WA TIMU RUWAWAZI BAADAYA KUIBUKA MABINGWA KOMBE LA MGOSI


MWENYEKITI WA SORUFA, HAMDANI HAMDANI KITANGAZA UTARATIBU WA KUTOA ZAWADI MBALIMBALI

SHABIKI

TIMU YA RED STARS ALIVAA JEZI YA JANO NA RUWAWAZI WALIVAA JEZI YA BLUU



PENALTI


PENALTI




Na Friday Simbaya, Peramiho


TIMU ya Ruwawazi kutoka Kata ya Lilambo imeibuka mabingwa baada ya.kuichapa Timu ya Red Stars ya Kata ya Peramiho mabao 6-5 kwa njia ya mikwaju ya penalti katika fainali ya Mashindano ya Kombe la Mgosi (Mgosi Cup 2012) yaliyofanyika Peramiho jana, Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

Awali timu hizo zilitoka sare ya kufungana mabao 2-2 katika ndani ya dakika 90 na baadaye kuijia moja kwa moja kipindi cha mikwaju, ambapo Red Stars ilikosa penalti mbili wakati Timu ya Ruwawazi ilipata penati zote.

Katika kipindi cha kwanza Timu ya Ruwawazi walipata bao la kwanza kupitia mshambuaji mchachali Geradi Steven dakika 21. Hadi kipindi cha kwanza kuisha Ruwawazi ilikuwa inaongoza 1-0.

Kipindi cha pili timu ya Red Stars ilirudisha goli mapema kupitia mshambuaji wake Basil dakika 58 na baadaye sana kuongeza goli la pili katika dakika 85 kupitia mshambuaji Edu. Kabla Red Star nao hawajakaa sawa sawa Ruwawazi walirudisha goli pili kupitia mshambuaji machachali Mobi Kangaluka dakika 87 kabla mpira kiisha.

Mwamuzi wa mechi ya fanali hiyo ya mashindano ya mgosi walikuwa ni Bw.Alfons Luoga wakati makamsaa walikuwa ni Bw. Milinga akisaidina na Bw. Mukoba.

Mashindano hayo yalianza mnamo tarehe 14.08.2012 na kumalizika 14.10.2012 na kushirikisha timu 10 kutoka kata za Peramiho na Lilambo, wilayani Songea, Mkoa wa Ruvuma, ambapo mdhamini wa mashindano hayo alikuwa mfanyabiashara mmoja wa Peramiho, Bw. Pascal Mgosi.


Akiongea na gazeti la mwenge mdhamini wa mashindano, Pascal Mgosi aliomba wadau wa mpira wa miguu pamoja na michezo mingine kujitoka na kudhamini michezo katika maeneo haya ili kuweza kukuza kiwango cha michezo na kuibua vipaji.

Aliongeza kuwa akiwa kama mfanyabiashara mdogo wameweza kudhamini mashindano hayo kwa nini isiwezekane hata kwa wadu wengine?, alihoji Mgosi.


Hata hivyo Bw. Mgosi aliseam kuwa malengo ya mashindano hayo ni pamoja na kukuza na kuboresa michezo kwa vijana wa kiume na wakike, kupunguza uzururaji, kupunguza tabia mbaya hasa za maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) yanayotokana ulevi wa kupidukia, kudumisha undugu na umoja na kuongeza kipato kupitia biashara ndogondogo wakati wa mashindano.

Kwa upande wa zawadi, mshindi wa kwanza aliibuka na kitita cha shilingi laki mbili (200,000/-) ambao ni Timu ya Ruwawazi FC, mshindi wa pili alijipatia shilingi laki na nusu (150,000/-) ambao ni timu ya Red Stars na ushindi wa watatu ulikwenda kwa Timu ya Mwanamonga FC kutoka pia Kata ya Lilambo, kwa kupata kifuta jasho cha 50,000/-.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...