Skip to main content

YANAYONIKERA: UPENDELEO KATIKA SEHEMU ZA KAZI!

Na Mwandishi Wetu
Kwa wale ndugu zangu hasa wa kuajiriwa na watu binafsi au na mashirika yasiyo ya serikali kama vile ya kidini na mengineyo hii inaweza kuwa imekutokea au umeishuhudia mwajiriwa mwenzio akitendewa.
Suala la upendeleo makazini si suala geni sana kwa asasi zisizo za kiserikali, upendeleo huu ambao mabosi huwafanyia baadhi ya watu fulani katika kampuni au shirika, kwa matakwa yao, kujipendekeza au kwa vigezo vingine visivyo vya maana. Watu hao wachache hupewa nafasi hizo za upendeleo kuliko wengine.
Nafasi hizo ni katika nyanja mbalimbali mfano, vipaumbele katika elimu na mafunzo mbalimbali, safari zenye posho, ruhusa pindi wana-pohitaji, upendeleo katika mishahara na mengineyo mengi ili kuwafurahisha watu hao makazini.
Kwa kawaida hali hii huwanufaisha sana watu hawa wachache ambao ni pendeleo la mwajiri (nyota ya bosi) kwani, vipaumbele hivyo huwa na manufaa sana kwao, lakini hali hiyo huwa kinyume kwa waajiriwa wengine pindi wanapobaini kuwa kuna ubaguzi wa namna fulani katika maeneo yao ya kazi.
Kuna mifano mingi ya hali za ubaguzi na upendeleo makazini, ila nilipoguswa na kukerwa leo ni upande wa mabosi kupanga mishahara jinsi wanavyojisikia bila kuzingatia majukumu ya wafanyakazi hao na vigezi vingine vya muhimu kama elimu na muda wakutumika katika kampuni kama ilivyo kwa asasi za serikali ambako wao hutumia viwango halali kwa vigezo maalumu(TGS Scale). Utakuta katika Kampuni wafanyakazi wameajiriwa kwa muda mmoja na wanakiwango cha elimu kina-cholingana na wanafanya majukumu ya aina moja cha ajabu na cha kushangaza unakuta wanalipwa mishahara tofauti, hali hii inakera sana.
Kwani mfanyakazi anayelipwa kawaida hatoweza kuwa na moyo wa kazi, na yule anayelipwa zaidi kuliko wengine kujiona bora zaidi, cha kushangaza utakuta majukumu anayoyafanya ni ya kawaida ukilinganisha na majukumu yanayofanywa na wafanyakazi ambao wanalipwa mishahara ya kawaida.
Upendeleo makazini unakera sana, kwani unamfanya mfanyakazi kujiona mnyonge na asiye na thamani, na hali hii inampunguzia mfanyakazi uwezo wa kufikiri mambo ya kuinufaisha kampuni au shirika, kwani mara zote atakuwa anafikiria kwa nini anabaguliwa au kwanini hasikilizwi.
Hali ya upendeleo makazini hupelekea waajiriwa wasiopewa vipaumbele kupunguza ari ya utendaji kazi kwa kuona kuwa kazi zao hazithaminiwi na kuoekana kama wanamchango mdogo katika Kampuni kutokana na matabaka mwajiri anayokuwa ameyatengeneza kwa dhima ya upendeleo katika uongozi na utawala wake.
Hali ya kupungua kwa ushirikiano na mara zote huathiri kampuni kwani wafanyakazi hufanya kazi kwa kusukumwa na si kwa kuipenda tena kutokana na hali hiyo ya kubaguliwa na upendeleo miongoni mwao.
Nini kifanyike sasa, ili kupunguza madhara haya katika sehemu za kazi, waajiri wanatakiwa kuwa na sababu za msingi na za kuridhisha za kutoa nafasi hizo za upendeleo kwa wafanyakazi na pia kila mfanyakazi afanywe sawa na wengine iwapo hasa kama ana vigezo vinavyolingana na kupata upendeleo huo.
Hivyo basi waajiri badilikeni fanyeni yaliyo haki na punguzeni mambo ya upendeleo usiokuwa na sababu zenye mashiko. Ili kazi ifanyike vizuri mnahitajika kufanya mambo yakuwaunganisha wafanyakazi wenu na si kuwajengea matabaka yasiyo ya msingi na kwa vigezo vya kipuuzi.
JUA SHERIA TENDA HAKI!

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...