Skip to main content

VIJANA ZAIDI YA 1600 KUAJIRIWA

Na Friday Simbaya


KAMPUNI inayojishughulisha na uchimbaji wa madini ya Urani ya Mantra Tanzania Ltd iliyopo Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma imesema itatoa ajira kwa vijana zaidi 1600 kutoka vijiji mbalimbali baada ya kupatiwa kibali cha kuanza kazi ya uchimbaji.


Hayo yamebainishwa hivi karibuni na Mjeolojia Mkuu kampuni hiyo Bw. Emmanuel Nyamusika wakati alipokuwa akitoa taarifa mbalimbali kwa waandishi wa habari wa mkoa wa Ruvuma (RPC) walipotembelea eneo la mgodi wa madini hayo kwa lengo la kujiridhisha baada ya kupata malalamiko kutoka vijijini vilivyo jirani mgodi huo.


Alisema,licha ya kutoa ajira hizo kwa vijana,kampuni hiyo imeshaanza kutekeleza kwa vitendo agizo la serikali ya awamu ya nne kwa kuwahamasisha wakazi wa vijiji jirani na mgodi huo kuanzisha vikundi vya kiuchumi na tayari imeshaanza kutoa fedha za kuwawezesha wanavikundi hao kuifanya shughuli za maendeleo kama ufugaji wa kuku wa mayai na nyama.

Alisema,lengo la kufanya hivyo ni kutaka wananchi hao kunufaika na uwepo wa mgodi huo na pia kuunga mkono juhudi za serikali.

Alisema, mpaka sasa bado wanaendelea na kazi ya utafiti kwa eneo lote lilokusudiwa ambalo ni km za mraba 332, lakini wameshindwa kufanya utafiti wao kwa eneo lote ilo kwa sasa na kufanikiwa kufanya utafiti wao kwa km za mraba 100.

"Tunategemea kuendelea na utafiti katika maeneo yaliyobaki baada ya kupata kibali cha kazi ya uchimbaji,lengo letu ni kutaka kuyafikia maeneo yote ya mradi huu,hata kuongeza ukubwa wa eneo kwani tunaamini pori ili lina hazina kubwa ya madini ya Urani,"alisema,

Pia ameiomba serikali,kusaidia upatikaji wa kibali cha uchimbaji ili waanze kutekeleza baadhi ya mipango yake ikiwemo ya ujenzi wa nyumba za watumishi katika vijiji jirani na eneo la mgodi kwa kuwa hairuhusiwi mtumshi kuishi kambini na familia yake.

Akizungumzia kuhusu uharibifu wa mazingira, Bw.Nyamusika aliwatoa shaka waandishi wa habari kusema kuwa watakuwa na utaratibu wa kufukia mashimo hayo ,na kupanda nyasi na baadhi ya mimea itakayosaidia kurudisha maeneo hayo katika hali yake ya kawaida.
Ziara ya waandishi wa Mkoa wa Ruvuma (Ruvuma Press Club) kwenye mradi wa Mkuju River Project ulifanyika tarehe 8/12/2012. Mradi huo hupo umbali wa zaidi kilemeta 50 kutoka Kijiji cha Likuyu Sekamaganga.

Hata hivyo, ziara ya waandishi wa habari kwa kampuni ilikuwa na lengo la kuhufahamu mradi wa Mkuju River Project; kujifunza kuhusu madini ya urani na vifaa vya mionzi na mahusiano kati ya jamii zilizopo na kampuni.




Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Ruvuma Press Clubu ,Andrew Kuchonjoma alimshukuru Mantra Tanzania Limited pamoja uongozi wa Wilaya ya Namtumbo kwa niaba ya waandishi wa habari kwa kuandaa ziara, na alisema ziara ilikuwa na mafanikio.

"Tumepata elimu juu ya ukweli kuhusu vifaa vya madini ya urani na mionzi na dhana potofu kuhusiana mradi Mkuju River Project. Wote tunahitaji ni kwenda nyumbani na kujaribu kuelimisha jamii katika maeneo yetu kuhusu ukweli wa urani, "alisema Kuchonjoma.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...