Skip to main content

WANACHAMA 150 WA CCM PERAMIHO WATIMKIA CHADEMA



Na Friday Simbaya, Songea
Jumla ya wanachama 150 wa Chama cha Mapinduzi (CCM), vijana kwa wazee wa Kata ya Peramiho wamekata shauri na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kati yao 130 wamerudisha kadi za CCM na wengine 20 ni wanachama wapya, wakati wa mkutano wa hadhara  uliofanyika eneo la Namihoro sokoni, Wilaya ya Songea (V) mkoani Ruvuma juzi.

Kada na mpigadebe wa CCM maarufu, Margret Ndomba (kushoto) akipeana mkono na Mjumbe wa Kamati Kuu Taifa (NEC CHADEMA), Edson Mbogolo baada aliyakurudisha kadi tatu za CCM, yaani kadi ya UVCCM, kadi ya UWT na CCM wakati wa mkutano wa hadahra wa chama hicho uliyofanyika Namihoro katika Kata ya Peramiho Wilaya Songea, Mkoani Ruvuma juzi.


Miongoni mwa wanachama waliorudisha kadi za CCM na kuamua kujiunga na Chadema ni Mwenyekiti mstaafu wa CCM wa Tawi la Peramiho, Bruno Mwitumba pamoja na kada wa CCM Margret Ndomba aliyerudisha kadi tatu; kadi ya UVCCM, kadi ya UWT na CCM.

Akiwakabidhi na kuwapokea wanachama hao, Mjumbe wa Kamati Kuu Taifa (CHADEMA), Edson Oswald Mbogolo alisema kuwa wanachama hao waliohamia Chadema wamefanya hivyo kwa maamuzi sahihi kwa kuchagua maendeleo, na kuongeza kuwa wameamua kutoka ‘analojia kwenda digitali.’

“Wananchi hawa waliojiunga na Chadema kwenda ‘digitali kutoka analojia’ kwa maana ya kutoka CCM kwenda Chadema kama nchi yetu na nchi za Afrika Mashariki mzima ilivyoamia digitali wanajitambua…”, aliongeza Edson Mbogoro.

Alisema kuwa mwaka 2014 utachukuliwa kama ni mwaka wa Chadema na kipimo tosha cha kuchukua dola katika chaguzi za serikali za mitaa kwa nafasi mbalimbali katika ngazi zote na hatimaye Uchaguzi Mkuu 2015.

Alidai kuwa wananchi wa Kata ya Peramiho wameamua kujiunga na Chadema kwa sababu Mbunge wao wa Jimbo la Peramiho, Jenister Mhagama amewatelekeza.

Aliwambia wakazi wa Jimbo la Peramiho kujiunga na Chadema ili waweze kuunganisha nguvu kwa pamoja kuondoa watawala pamoja na mbunge wa jimbo hilo.

“Ndugu zangu wanaPeramiho siasa sio usanii kama wanavyofanya kina Majuto kumbe siasa ni uhai wetu, siasa ni maisha yetu…” alisisitiza mjumbe huyo wa kamati kuu taifa.

Naye Katibu waChadema Wilaya ya Songea Mjini, Masumbuko Mbogolo alisema kuwa wananchi  wake kwa wanaume wa Jimbo la Peramiho kuwa wanabudi  ya kuchagua upinzani kwa maendeleo ya jimbo lao, kwa sababu kwa muda mrefu jimbo hilo liko nyuma kimaendeleo.

Alisisitiza kuwa mahala ambapo wananchi wamechagua upinzani pana maendeleo kwa kutoa mifano michache ya Moshi mjini, Karatu  na Kijiji cha Liweta ambacho kipo kilometa chache kutoka Peramiho, ambacho kina maendeleo kwa sasa baada ya kuchagua upinzani na mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho ni wa Chadema.

“Kijiji cha Liweta ambacho kipo kilometa chache kutoa hapa Peramiho waliamua kuchagua upinzani baada ya miaka mingi ya kutawaliwa na CCM, kwa sasa wananchi wa kijiji hicho wana maendeleo, wamepata maji safi na salama baada ya kuchimbiwa visima, wamechongewa barabara na wanasubiri kujengewa zahanati kutokana na kelele za Chadema,” alisema Masumbuko Mbogolo.

Kuhusu mbolea, Katibu wa Wilaya ya Songea Mjini alisema kuwa wananchi wa Jimbo la Peramiho na kwingineko hawawezi kuwa na kilimo chenye tija kwa sababu gharama za pembejeo na mbolea ziko juu ukilinganisha na Malawi na Zambia wakati wote wanaagiza mbolea hizo kutoka China na Japan.

Alitoa mfano kuwa, kule Malawi mfuko moja wa mbolea unauzwa shilingi elfu nane tu wakati Tanzania mfuko mmoja wa mbolea unauzwa kati ya shilingi elfu 65 hadi 70, wakati Malawi na Zambia wanapitisha mbolea kupitia Tanzania na wanalipa kodi kwa Tanzania kwa kupitisha mizigo yao.

Katika hatua nyingine, Katibu huyo wa Wilaya ya Songea Mjini alipata nafasi ya kufafanua maana ya rangi nne za bendera ya chama hicho (Chadema) kwa wananchi wa Jimbo la Peramiho.

 Alifafanua kuwa rangi nyeupe kwenye bendera ya chama hicho ni alama na ishara ya amani, rangi nyeusi katika bendera hiyo ni alama ya watu, rangi ya Bluu inaonyesha alama ya utajiri wa asili wa nchi ya Tanzania  na rangi nyekundu ni alama ya damu iliomwagika kutoka kwa baadhi ya wapigania Uhuru wa nchi hii kama vile Mkwawa na wengineo.

Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...