Skip to main content

MAAMUZI YA MFADHILI WA KOMBE LA ANSGAR 2013 (SOKO)



Na Friday Simbaya, Songea

Mwenyekiti wa Kamati ya waratibu wa Mashindino ya Kombe la Ansgari
2013, Emeran Ndunguru akisoma taarifa ya maamuzi yao kuhusu kufutwa
kwa michezo ya mpira ya miguu kwa mshindi wa tatu na fainali leo.

Kamati ya mashindano ya Kombe la Pasaka (Ansgar Cup) Tarafa ya Ruvuma,
Wilaya Songea (V) mkoani Ruvuma hatimaye imefuta fanaili michezo ya
mpira wa miguu kwa mshindi wa tatu na fanaili kwa mwaka huu kutokana
na malumbano yanayoendelea  kati ya timu za Kilagano na Peramiho B,
yaliyoanza wakati nusu fainali.

Akiongea na waandishi wa habari leo (Alhamisi) mwenyekiti wa kamati,
Emeran Ndunguru alisema,  malumbano hayo yamepelekia  kufutwa kwa
fanaili hizo michezo wa mpira wa miguu ni kati ya  timu ya Kilagano na
Peramiho B, ambapo Kilagano walidai kuwa timu ya Peramiho B
ilichezesha baadhi ya wachezaji ambao ni mamluki l wakati wa  mchezo
ya nusu fanaili uliyofanyika katika Uwanja wa Nanenane, Kijiji cha
Mgazini katika Kata ya Kilagano wilayani Songea.

Emeran Ndunguru anayefanya kazi ya ufadhili pamoja na kamati yake
badala ya mfadhili Dr. Ansgar Stuffe, alisema michezo ya mpira wa
miguu kwa mshindi wa tatu  na fainali imefutwa ili kuwapa nafasi zaidi
kuendelea na malumbano hadi ukweli ujulikane.

Alisema kuwa wakati vilabu hivyo vya mpira wa miguu vikiendelea
kulumbana, fainali za mpira wa pete (Netball) na mshindi wa tatu
zitafanyika tarehe 16.06.2013 siku ya Jumapili katika Uwanja wa Ansgar
Peramiho.

Mfadhili wa Kombe la Ansgar ni Dr. Ansgar Stuffe OSB, mkurugenzi wa
Hospitali ya Peramiho aliamua kuwepo na michezo katika vijiji vya
Peramiho, shule za msingi za Peramiho na baadaye michezo ilipanuka
hadi tarafa ya Ruvuma.

“Michezo hii imechezwa kwa mafanikio zaidi ya miaka kumi na tano (15),
na ushindi umekuwa wa kupokezezana kata hadi kata hapakutokea usumbufu
kama huu wa kulumbana kati ya vilabu na vyama vya michezo yaani SORUFA
na FARU. Kama waratibu chini ya mfadhili hatuelewi nguvu ya malumbano
hayo yanatoka wapi!,” alishangaa Ndunguru.

Mwaka huu michezo ilianaza kwa ushindani mkali huko Kata ya Kilagano,
ambapo mashindano hayo yanashirikisha kata za Mpandangindo, Peramiho

,Litisha na Kilagano (wenyeji), tarafa ya Ruvuma wilayani Songea
Vijijini.

Mashindano haya yanadhaminiwa na Dr. Ansgar Stuffe OSB, Mkurugenzi wa
Hospitali ya Peramiho ambayo yalianza tarehe 21.04.2013 na
yalitarajiwa kuamalizika Siku ya Ekaristi Takatifu mnamo tarehe
02.06.2013.

Mashindino ya Kombe la Pasaka (Ansigar Cup) Tarafa ya Ruvuma (Soka na
Pete) yanafanyika kwa mara ya kwanza katika Kata ya Kilagano katika
Kijiji cha Mgazini, ambapo miaka yote mashindano hayo yalikuwa
yanafanyika katika kata ya Peramiho.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...