Skip to main content

JKT MLALE YAIBAMIZA MAJIMAJI FC MAGOLI 2-0



Mwenyekiti wa Timu ya Majimaji Hamphrey Milanzi (kushoto) na Kocha ya timu  hiyo Peter Mhina wakifuatilia mchezo kwa umakini kati  ya timu yao na JKT Mlale  uliofanyika katika Uwanja wa Majimaji mjini Songea, mkoani Ruvuma leo, ambapo JKT Mlale ilishinda magoli 2-0. (Picha na Friday Simbaya)







Na Friday Simbaya, Songea

 JKT  MLALE imeiadhibu timu ya Majimaji ya Songea mjini bila huruma kwa kuibamiza magoli 2-0 katika michuano ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inayoshirikisha timu 24 zilizogawanywa katika makundi matatu msimu huu, iliyoanza kutimua vumbi Septemba 14, mwaka huu.

Mechi ya ufunguzi ya timu hizo mbili zilifanyika katika Uwanja wa Majimaji mjini Songea mkoani Ruvuma, huku wenyeji Majimaji FC wamechapwa magoli 2-0 na timu ya JKT Mlale.

Aidha, JKT Mlale ilipata goli la kwanza kupitia mshambuliaji wake Edward Songo mnamo dakika 19 katika kipindi cha kwanza na goli la pili lilifungwa na Ally Bilali dakika ya 21.

 Kila timu itakayoongoza kundi lake katika ligi itakayochezwa kwa mikondo miwili (nyumbani na ugenini) ndiyo itakayopanda daraja kucheza Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2014/2015.

 Kwa mujibu wa taarifa ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), mechi za ufunguzi kwa kundi A zitakuwa kati ya Tessema dhidi ya Green Warriors (Uwanja wa Karume, Dar es Salaam) wakati Septemba 15, mwaka huu ni Transit Camp itakayocheza na Polisi Dar (Uwanja wa Mabatini, Pwani).

Mechi nyingine siku hiyo ni Ndanda itakayoivaa Friends Rangers (Uwanja wa Nangwanda, Mtwara) wakati Villa Squad itaikabili African Lyon itachezwa Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

 Kundi B ni Burkina Faso itacheza na Polisi Moro (Uwanja wa Jamhuri, Morogoro), Mkamba Rangers itaivaa Lipuli (Uwanja wa CCM Mkamba, Morogoro), Majimaji itakuwa mwenyeji wa Mlale JKT (Uwanja wa Majimaji) wakati Septemba 15, Kimondo SC itacheza na Kurugenzi (Uwanja wa Sokoine, Mbeya).

 Mechi za ufunguzi kundi C ni Polisi Mara dhidi ya Polisi Dodoma (Uwanja wa Karume, Musoma), Kanembwa JKT itacheza na Polisi Tabora (Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma), Stand United itaivaa Mwadui (Uwanja wa Kambarage, Shinyanga), na Pamba dhidi ya wenzao Toto Africans (Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza).

 Taarifa ya TFF ilisema kuwa mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo utamalizika Oktoba 26, mwaka huu wakati wa pili utamalizika Machi 22, mwakani.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...