Skip to main content

MASHINDANO YA KOMBE LA ANSGARI (ANSGAR CUP) MWAKA 2014 YANUKIA

Dkt Ansgar

Mashindano ya Kombe la Ansgar (Ansgar Cup) tarafa ya Ruvuma, wilayani Songea vijijiin, mkoani Ruvuma yanatarajia kutimua vumbi katika viwanja vya Ansgari vilivyopo Peramiho kuanzia tarehe 13/04/2014 na kumalizika 22/06/2014 Siku ya Ekaristi Takatifu, imefahamika.


Akitangaza ratiba hiyo Kaimu Mwenyekiti wa Mfadhili, Dkt. Magnus Mwanyika wakati kikao cha maandalizi ya mashinadano hayo kulichofanyika jana eneo la Mgahawa wa Peramiho, alisema kuwa mashindano hayo yataanza tarehe 13/04/2014 ngazi ya kata na fainali ngazi ya tarafa yatafanyika siku ya Ekaristi Takatifiu tarehe 22/06/2014.


Dkt. Mwanyika aliwaambia wajumbe kamati ya maandalizi kuwa mwaka kutakuwa na mabadilko kidogo kwa upande wa zawadi , ambapo alifafanua kuwa mshindi wa kwanza atapata zawadi ya 300,000/- (futiboli na netiboli), wa pili ataondoka na shilingi 250,000/- na mshindi wa tatu atajipatia 150,000/- (mpira wa miguu na pete) ukilinganisha na mwaka jana.


“Zawadi mwak huu zimepanda kutoka 250,000. hadi 300,000/- kwa mshindi wa kwanza, mshindi wa pili vile vile mwaka huu atapa shilingi laki mbili na nusu toka laki moja na nusu na wa tatu vile vile atajipatia shilingi laki moja na nusu toka shilingi laki moja,” alsiema mwenyekiti huyo.


Alisema kuwa katika ngazi ya kata, zawadi zitakazotolewa ni kwa mshindi wa kwanza na pili tu, ambapo mshindi wa kwanza atapewa shilingi elfu sabini na mshindi wa pili atapaiwa shilingi elfu hamsini kwa mipra wa miguu na pete (Netiboli).


Aliongeza kuwa katika mashindano ya mwaka huu pia kutakuwa na zawadi ya mfungaji bora (best Player) wakati wa fanaili.

“Mfadhili atatoa mipira miwili miwili kwa kila timu itakayoshirika mashindano ya Ansgari mwaka 2014, yaani futuboli na netiboli, mpira moja moja, ngazi ya kata” alifafanua Dkt. Mwanyika.


Kwa upande wa usafiri, Kaimu Mwenyekiti wa Mfadhili alisema kuwa atatoa shilingi laki moja moja kwa timu za Kilagano na Mpnadangindo kutokana na umbali kata hizo ukilinganisha na timu zingine za tarafa ya Ruvuma.


“Kata zingine zitachangiwa shilingi elfu sabini kwa ajili ya kufanyikisha usfari kwa timu zitakazo cheza fainali katoka katani hadi kwenye viwanja vya mashindano,” alisema Dkt. Mwanyika.


Katika hatua nyingine, Kamati ya Maandalizi imemchagua Joseph Mbunda ambaye pia ni Mratibu Elimu Kata ya Maposeni kuwa mwenyekiti mpya baada ya aliyekuwa mwenyekiti Ayubu Mvula kuhamia katika tarafa nyingine nje ya tarafa ya Ruvuma, wakati kwa upande wa katibu, Sixbert Komba ameendelea kushika nafasi ili ile ya ukatibu mpaka mwisho wa mashindano.

Wakati huohuo, Kaimu Afisa wa michezo wa Wilaya ya Songea, Moses Kipanga alizitaka timu zote zitakazoshiriki mashindano mwaka huu kufanya usajili kama sheria ya michezo nchini inavyoelekeza pamoja na kuwa katiba zao.

Alisema kuwa mwaka huu utaratibu umebadilika timu zote zitakazoshiriki mashindano ina lazimika kufanya usajili katika ofisi ua usajili wa vilabu ya wilaya ili kuepuka udanganifu kama wa mwaka jana, ambapo timu nyingi zilikuwa hazina usajili na katiba.

MALENGO YA MASHINDANO

Mashindino hayo hufanikishwa chini ya ufadhali na udhamini wa Mkurugenzi wa Hospitali ya Peramiho Dr. Br. Ansgar Stüfe OSB na kuratibiwa na uongozi wa michezo wa hospitali hiyo. Mashindano huendeshwa kwa kufuata sheria za michezo nchini.

Uendeshaji hufanywa chini ya waheshimiwa madiwani wa tarafa, watendaji wa kata na waratibu wa elimu wa kila kata katika Tarafa ya Ruvuma.

Malengo ya mashindano hayo ni pamoja na kukuza na kuboresha michezo kwa vijana wa kiume na wa kike wa Tarafa ya Ruvuma, kupunguza uzururaji, tabia mbaya hasa za maambukizi ya Virusi vya Ukimwi, kudumisha undugu na umoja wa kitarafa na kuongeza kipato kupitia biashara ndogondogo wakati wa mashindano.

Mashindano hayo yalishirikisha kata tano za tarafa ya Ruvuma ambazo ni Maposeni, Mpanda-ngindo, Peramiho, Litisha na Kilagano.







Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...