Skip to main content

SHULE YA PERAMIHO GIRLS YAONGOZA KIMKOA MATOKEO KIDATO CHA NNE



Na Friday Simbaya, Songea
Wakati Shule ya St. Francis Girls ya Mbeya ikishika nafasi ya kwanza kitaifa, nayo Shule ya Peramiho Girls ya Ruvuma imeibuka kidedea kwa kushika nafasi ya kwanza kimkoa pia katika matokeo ya kidato cha nne 2013, imefahamika.
Katika uchunguzi waliofanya na MWANDISHI WA MWENGE, ulimebaini kuwa Shule ya Wasichana Peramiho ya wilayani Songea vijijini, mkoani Ruvuma imeshika nafasi ya kwanza kimkoa kati jumla ya shule 113 na kushika nafasi 21 kitaifa kati jumla ya 3256 nchini.
Akizungumza na Mkuu wa Shule, Bi. Lucida Msabila alisema kwamba alikuwa na uhakika wa shule yake kufanya vizuri kutoka na maandalizi mazuri waliopata wanafunzi wa shule hiyo katika masomo.
Akielezea siri ya mafankio hayo Msabila alisema shule yake ilifanya vizuri kutokana ushirikiano mzuri ulipo kati ya wanafunzi, walimu na wazazi, ambapo mwaka 2012 lifanikiwa  kushika nafasi ya pili kimkoa.
“Siri ya mafanikio nikujipanga tu kutoka mwanzo pamoja na kuwa na mpango kazi kwa kuhakikisha Walimu wanafundishia masomo na kama Mwalimu hakumalizi masomo ni lazima afundishe muda wa wikiendi ili kufidia vipindi walivyoruka..” alisema Msabila.
Alisema kuwa mwaka jana shule hiyo ilishika nafasi ya pili kimkoa lakini kitaifa matokeo ya kidato cha nne yalikuwa mabovu, na kuongeza kuwa katika matokeo ya kidato cha nne mwaka huu hakuna mwanafunzi aliyepata sifuri na daraja nne lakini kuna mwanafunzi moja tu aliyepata daraja la tatu.
Shule ya Wasichana ya Peramiho pamoja na mafankio pia zipo changamoto kama vile upungufu wa vitabu vya uraia, historia, jeografia na fizikia pamoja na utitiri wa vitabu ambayo unawapashida kipi kutumike.
“Changamoto nyingine ni wanafunzi wengi hawapo tayari kusomo kwa hivyo kama uongozi wa shule tunalazimika kuwasimamia kwa ukaribu…” alielezea Msabila.
Shule hiyo ya Peramiho girls ambayo inamilikiwa na masista wa Mtakatifu Scholastica (Missionary Benedictine Sisters of Tutzing) ilianza mwaka 1968, na Lucida Msabila ni mwalimu mkuu wa 13 tangu 2004 mpaka sasa.
Hata hivyo mkuu huyo
aliponda mfumo mpya wa upangaji matokeo kuwa hautaonesha uhalisia ya mwanafunzi kufanya vizuri ukizingatia kwamba tupo katika jumuiya ya Afrika mashariki na hawata himili ushindani wa soko la ajira la kimataifa hapo baadae.
Shule hiyo imetoa viongozi wengi wa kitaifa wakiwemo spika wa bunge wa sasa Anna Makinda na naibu Waziri wa elimu wa sasa Jenister Mhagama.
Hivi karibuni Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), lilitangaza matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne 2013, huku ufaulu ukiongezeka kwa asilimia 15.17. Matokeo hayo ni ya kwanza kutumika kwa mfumo mpya ambao umepanua wigo wa alama na madaraja, hivyo kutoa nafasi zaidi kwa watahiniwa kufaulu.
Akitangaza matokeo hayo jijini Da er Salaam Kaimu Katibu Mtendaji, Dk. Charles Msonde alisema waliofaulu mtihani ni 235,227 sawa na asilimia 58.25 ya 404,083 ya waliofanya mtihani huo, ukilinganisha na 185,940 mwaka 2012, sawa na asiliamia 43.08.
Dk. Msonde alisema matokea haya yalipangwa kwa kutumia alama zilizotangazwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome mwaka jana.
Alama hizo ni A: 75-100, B+: 60-74, B: 50-59, C: 40-49, D: 30-39, E: 20-29 na F: 0-19. Kabla ya mabadiliko hayo, alama zilizokuwa zinatumika kupanga matokeo ya kidato cha nne ni A: 80-100, B: 65-79, C: 50-64, D: 35-49 na F: 0-34.
Dk. Msonde alisema wasichana waliofaulu ni 90,064 sawa na asilimia 55.49 na wavulana ni 111,088 sawa na asilimia 58.45.
Mwisho


Mkuu wa Shule Sekondari ya Wasichana Peramiho Lucida Msabila.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...