Skip to main content

MAMIA YA WAKAZI WA PERAMIHO WAMZIKA BABA MZAZI WA RAIS WA VICOBA TANZANIA



Na Friday Simbaya, Songea
Paroko Msaidizi wa Parokia ya Peramiho katika Jimbo Kuu la Songea, Padre Benedict OSB ametoa rai kwa wazazi wa Peramiho na kwingineko kuwaelekeza watoto katika masomo kwa sababu elimu ni mwanga wa maisha.
Alisema kuwa wazazi na walezi wanapaswa kuwasomesha watoto wao ili kuwaandalia maisha mazuri kwa baadaye yenye faraja.
Paroko huyu aliyasema haya jana wakati wa Ibada ya Misa Takatifu ya mazishi ya marehemu Barnabas Jacob Mkuwa (91), ambaye alikuwa baba mzazi wa Mbunge wa Viti Maalum, Rais wa Vicoba Tanzania na Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Devote Mkuwa Likokola.
Misa hiyo iliyofanyika nyumbani kwa marehemu Mtaa wa Madukani, Peramiho wilayani Songea, mkoani Ruvuma iliongozwa na mapadre saba, akiwemo Padre Lucius OSB aliyeongoza madhehebu yote ya Misa.
Alisema kuwa kuna baadhi ya wazazi wanakwepa majukumu ya kuwalea watoto wao katika maadili mema ikiwa pamoja na kuwapatia elimu, afya, mavazi na malezi. “Watoto ni zawadi kwenu, simameni imara katika malezi ili baadaye wawe faraja kwenu,”aliongeza paroko huyo.
‘Wazazi na walezi popote duniani wanatambua kuwa hakuna jukumu zito kama la kulea watoto. Ni kazi ngumu ambayo haina likizo. Wazazi makini huwalea watoto wao kwa kuwapatia elimu, afya, mavazi na malezi,’alisema paroko huyo.
Alitoa mfano wa marehemu Barnabas Jacobo Mkuwa walifanya kazi  vizuri ya malezi kwa kuwasomesha watoto wake wote, ndiyo maana aliishi maisha marefu yenye faraja kwa sababu ya kuwapatia elimu watoto wake.
Aliongeza kuwa wazazi wa jana, leo na kesho wakumbuke kuwa kazi ya malezi ni jukumu la uhai wote, hivyo basi wazazi wakumbuke kuwa samaki mkunje angali mbichi, kwa sababu jinsi watakavyo walea watoto wangali wadogo ndivyo watakavyofarijika zaidi baadaye na kuyaona matunda mema ya watoto wao.
Kwa upande wake Fr. Lucius OSB ambaye pia Priori Mstaafu wa Abasia ya Peramiho kwa niaba ya jamii ya Abasia ya Peramiho alitoa shukurani  kwa ukoo wa familia ya Mkuwa kwa kutoa mchango mkubwa kwa  kuendeleza umissionari  hapa Peramiho tangu kuanzishwa kwake miaka 114.
Alisema kuwa ukoo wa Mkuwa ulikuwa bega kwa bega kwa kuhakikisha maendeleo ya Abasia ya Peramiho kwa hakikisha kuwa umisionari hapa Peramiho unakuwa na kusimama imara.
Wakati huohuo, wabunge wa Mkoa wa Ruvuma kwa kupitia mwenyekiti wa wabunge wa Mkoa wa Ruvuma, Jenister Mhagama wametoa rambirambi ya shilingi laki tisa (900,000/-) kwa mbunge mwenzao, Devote Likokola kwa kufiwa na baba yake mzazi.
Marehemu Barnabas Mkuwa alizaliwa tarehe 23.04.1923 hapa Peramiho, ameacha watoto saba wote wakike, wajukuu 36 na vitukuu 31. Alifariki dunia tarehe 13.03. 2014 katika Hospitali ya Mtakatifu Joseph Peramiho kwa ugonjwa shinikizo la damu na kuzikwa katika makaburi ya Namihoro Peramiho.
Marehemu Barnabas alibatizwa tarehe 27.04.1923, alipata Kumunio ya Kwanza tarehe 25.06.1931. Kipaimara tarehe 28.05.1934 na alifunga ndoa na Isabella Mukaranga ambaye pia ni marehemu mnamo tarehe 10.06.1943 katika Kanisa la Peramiho.
Alianza kazi ya ualimu mwaka 1942 na kustaafu  mwaka 1978 ambapo wakati wa uhai wake alifundisha shule mbalimabli za msingi zikiwemo Likuyufusi, Ndilima, Namabengo, Lilambo, Parangu, Mtyangimbole, Tukuyu, Liganga, Lipaya na Peramiho zote za Mkoa wa Ruvuma.
Mwisho











Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...