Skip to main content

UKAWA: TUTAIDAI TANGANYIKA NJE YA BUNGE


Zanzibar. Viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wameapa kuendelea kudai mfumo wa Muungano wa serikali tatu nje ya Bunge la Katiba kwa nguvu zote, ikiwamo kufanya maandamano ya amani nchi nzima.
Msimamo huo ulielezwa na viongozi hao kwa nyakati tofauti katika mkutano wa hadhara uliofurika mashabiki kwenye Viwanja vya Kibandamaiti, Unguja jana.
Mwenyekiti Ukawa, Freeman Mbowe alisema wameamua kuliacha Bunge la Katiba kutokana na harufu za rushwa, vitisho na matusi huku baadhi ya wabunge wakiahidiwa vyeo. Mbowe ambaye hata hivyo hakufafanua zaidi, alisema Ukawa wameamua kwenda kwa wananchi kuwaeleza dhamira chafu walionayo wabunge wa CCM katika mpango wao wa kukataa Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyowasilishwa na Jaji Joseph Warioba.
“Ni jambo la hatari katika mchakato wa Katiba wananchi kuwa waoga au hofu... Lazima tuwe tayari kuwaonyesha watawala kuwa tuna umoja imara, tunayapigania mataifa huru ya Tanganyika na Zanzibar, Rais Kikwete (Jakaya) asiwatishe wananchi kwa kivuli cha jeshi kuchukua madaraka,” alisema Mbowe.
Lipumba anena
Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, Profesa Ibrahim Lipumba alisema wajumbe wa Ukawa wameamua kujitoa bungeni kutokana na kauli ya Rais Jakaya Kikwete ambayo alidai kuwa iliibeza na kuidhalilisha Tume ya Warioba.
Alisema hawatarudi bungeni na kwamba hawawezi kujadili Katiba ambayo siyo maoni ya wananchi.
Alidai kwamba kwa makusudi Rais Kikwete aliamua kutetea sera za chama chake na kupingana na maoni yaliyotolewa na wananchi kupitia Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
“Rais Kikwete ameharibu nia ya kupatikana Katiba Mpya, amekuwa akijulishwa kila hatua na jinsi maoni ya wananchi walivyokuwa wakipendekeza serikali tatu katika Rasimu ya Kwanza na ya Pili naye akawa anaafiki, inashangaza amegeuka na kukataa maoni ya wengi,” alisema Profesa Lipumba.
Mtikila akumbushia jela
Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila alisema aliwahi kufungwa jela mara tatu, kuwekwa mahabusu mara 43 kwa kudai lipatikane Taifa la Tanganyika huku watawala wakikataa matakwa ya wengi kwa sababu na hoja dhaifu.
Mchungaji Mtikila aliongeza kusema kwamba wanachokitaka CCM na Serikali zake ni kuendelea kuwabana wananchi wa Tanganyika na Zanzibar wasiweze kuwa huru na kujivunia mataifa yao.
Seif: Mimi Ukawa damu
Akihutubia mkutano huo, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad alieleza msimamo wake kuwa anaunga mkono harakati hizo na yeye ni Ukawa damudamu.
“Walikuwa hawajui msimamo wangu, waelewe kwamba mimi ni Ukawa damu,” alisema.
Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, alisema wanaotetea mfumo wa serikali mbili ni sawa na watu wanaopigania kuendelea kuwapo kwa dhuluma Tanzania.
“Hatuwezi kuendelea na mfumo huu, tumekuwa tukipiga kelele kwamba Muungano huu wa serikali mbili umeteka mamlaka yetu,” alisema Maalim Seif. Alimtaka Rais Kikwete asiwatishe wananchi kwa sababu wamependekeza mfumo mpya wa serikali... “Unaposema kwamba jeshi litapindua nchi kama tukiwa na Muungano wa serikali tatu, unamaanisha nini kama Amiri Jeshi Mkuu?” alihoji Maalim.
Katika mkutano huo, ulinzi uliimarishwa vya kutosha huku magari ya FFU na vikosi vya SMZ yakiwa yameegeshwa pembeni na askari waliokuwa wamebeba silaha na mabomu viunoni wakilinda. (CHANZO: MWANANCHI) (FS)


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...