Skip to main content

ZITTO KABWE AGEUKA KIVUTIO MAZISHI YA BABAKE FILIKUNJOMBE LUDEWA

Kutoka  kushoto mkuu wa wilaya ya  Ludewa  Juma Madah ,mbunge wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe na mbunge wa jimbo la  kigoma kaskazani Zitto Kabwe wakiwa katika msiba wa babake Filikunjombe mjini Ludewa jana.


DC Ludewa Bw Juma Madaha akitambulisha  viongozi mbali mbali




Mbunge wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe kushoto  akilitazama jeneza lenye mwili wa babake marehemu  Frolian Filikunjombe likiingizwa  ndani ya kanisa la RC Ludewa kwa ajili ya ibada ya mwisho kabla ya mazishi  yaliyofanyika katika makaburi ya Ludewa mjini


Na Francis Godwin Blog 
MBUNGE  wa  jimbo la Kigoma Kasikazin Zitto (CHADEMleo amegeuka  kuwa  kivutio  kikubwa  katika mazishi ya babake mbunge wa  jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe huku wananchi  wa  jimbo  hilo na viongozi wa CCM mkoa  wa Njombe  wakimbebesha majukumu  ya ubovu wa barabara  kwa  kumtaka  kushirikiana na mbunge wao  kuwasha moto bungeni .
Zitto  ambae  katika msafara  wake  huo  aliongozana na mbunge wa  jimbo la Mwibara Kangi  Lugola (CCM) mbunge wa  viti maalum mkoa wa  Tanga Amina Mwidau (CUF) na  wengine wa CCM nusuru avuruge  msiba  huo baada ya  wananchi  kuonyesha  kuvutiwa na uwepo  wake na  kumtaka   kusikia  sauti  yake .
Awali  wakati wa utambulisho  wa  viongozi wa kitaifa  uliofanywa na mkuu wa  wilaya ya   Ludewa Juma Madaha  waombolezaji  baada ya  kusikia  jina la Zitto Kabwe  katika orodha ya wabunge hao ndipo  sauti  ziliposikika  kuwa  wanahitaji azungumze .
Hata hivyo  katika  salam  zake katibu wa itikadi na uenezi wa CCM mkoa wa Njombe Honoratus Mgaya mbali ya  kumpongeza  mbunge Kabwe kwa  kufika katika msiba   huo na timu  yake bado  alimtaka  Kabwe na timu  yake  kusaidiana na mbunge  wao Filikunjombe kupigania ujenzi wa barabara ya lami kati ya Ludewa na Njombe.
"Mheshimiwa  Zitto Kabwe wewe ni mmoja kati ya wapiganaji wa kweli  bungeni kama  alivyo mbunge  wetu na jembe  letu wana Ludewa  Deo Filikunjombe ....sasa tunaamini mmeona ubovu wa barabara ya Njombe - Ludewa hivyo  kupitia ninyi  sisi  wana Njombe na Ludewa  tunaomba msaidiane na Filikunjombe kupigania suala la ubovu wa barabara na sio  kutoka nje ya bunge pindi suala la ubovu wa  miundo mbinu linapotolewa na mbunge  wetu"
Kufuatia  ombi hilo la Mgaya  waombolezaji walilipuka kwa  furaha   huku Zitto  Kabwe  akionyesha kuguswa na ombi hilo na kumtania mbunge wa  viti maalum mkoa wa Tanga Amina Mwidau (CUF)  kuwa UKAWA hao .
Zitto Kabwe  ambae alikuwa ni mmoja wa abiria  waliosafiri pamoja na babake Filikunjombe mzee Frolian Filikunjombe kabla ya kufariki  dunia akiwa  ndani ya ndege  kutoka  Dubai kuja nchini ni  mmoja  wa   marafiki  wakubwa wa mbunge Filikunjombe na pia ni mwenyekiti wa kamati ya PAC ambapo  Filikunjombe ni makamu mwenyekiti wake.
Hata  hivyo  alisema  kuwa  ombi la  wana Ludewa  kwake atalifanyia kazi na  kuwa suala la siasa lina  sehemu yake na yanapozungumzwa mambo ya kimaendeleo siasa  za  vyama zinawekwa kando .
Hivyo  alisema  kuwa kutokana na mahusiano mema  kati yake ya mbunge Filikunjombe ameguswa na msiba  huo na kuwa pindi atakapofika  bungeni maombi ya  wana Ludewa atayatendea kazi . (FS)


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...