Skip to main content

PROGRAMU YA PANDA MITI KIBIASHARA YAANZA KUTEKELEZWA KATIKA WILAYA SITA


Moja ya kitalu cha kuotesha miche ya miti kilichopo katika kijiji cha Kifanya wilayani Njombe; kitalu hicho ni cha wakulima wanaounda umoja wa wapanda miti Kifanya
Meneja Mawasiliano wa Mradi, George Matiko akifafanua jambo kwa wanahabari; aliyeketi ni Mkurugenzi wa Programu hiyo, Dk Maria Tham
Dk Maria Tham katika mahojiano na wanahabari ndani ya ofisi zao zilizopo mjini Njombe
Mwenyekiti wa kikundi cha wapanda miti wa kijiji cha Kifanya akitoa ufafanuzi wa shughuli zinazofanywa na kikundi chao
PROGRAMU ya Panda Miti Kibiashara imeanza kutekelezwa katika wilaya mbalimbali za mikoa ya Iringa, Njombe na Morogoro.
Wilaya hizo kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Programu hiyo yenye makao yake makuu mjini Njombe, Dk Maria Tham ni pamoja na Makete, Njombe na Ludewa kwa mkoa wa Njombe.
Wilaya zingine ni Kilolo na Mufindi kwa mkoa wa Iringa na Kilombero kwa mkoa wa Morogoro.
Dk Tham alisema lengo kuu la program hiyo iliyoanza Januari mwaka huu ni kuongeza kipato vijijini kutokana na kupanda miti kitaalamu kwa kutumia mbegu bora na kuhudumia mashamba ipasavyo kwa kuzingatia mipango ya matumizi endelevu ya ardhi.
 “Uwezo wa kufikia lengo kuu la program ni mkubwa kwa kuwa katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kuna udongo unaofaa kukuza miti, mvua za kutosha, ardhi ya kutosha na wakazi wake wanapenda kupanda miti,” alisema.
Alisema kwa kupitia program hiyo mipango ya matumizi endelevu ya ardhi itatengenezwa huku wananchi wanaopanda miti wakihamasishwa kuunda vikundi vya wakulima wa miti kwa nia ya kufanikisha shughuli za upandaji miti.
Katika kipindi cha miaka minne kuanzia sasa wananchi katika wilaya hizo watahamasishwa kupanda miti katika eneo lenye ukubwa wa hekta 15,000.
“Huku wakihimizwa kuanzisha shughuli mbalimbali za kujiongezea kipato wakati wakisubiri miti yao ikue na kufikia umri unaofaa kuvunwa,” alisema.
Alisema biashara ya miti itaongezeka kwa kuzingatia kwamba ifikapo mwaka 2025 inatarajiwa mahitaji ya malighafi viwandani na kuni yataongezeka kutoka mita za ujazo milioni 1.5 hadi milioni 3.7.
Baadhi ya wakulima wasema wameupokea mradi huo kwa mikono miwili na wakaahidi kutoa ushirikiano ili malengo yake yafanikiwa kwa faida yao na Taifa kwa ujumla. (BONGOLEAKS)

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...