Skip to main content

SERIKALI YAZINDUA KAMPENI YA UPIMAJI VVU MAHALI PA KAZI

Katibu Mkuu Utumishi George Yambesi(kulia) akipewa ushauri nasaha kabla ya kupima VVU kwa hiari wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kuhamasisha Upimaji VVU Mahali pa Kazi uliofanyika mjini Njombe juzi
Akitoa nasaha zake kwa wawakilishi wa mikoa ya Iringa na Njombe walioshiriki uzinduzi wa kampeni hiyo
Hilda Kapanda mmoja wa watumishi wa halmashauri ya Njombe anayeishi na VVU akitoa ushuhuda wake

Huyu Anjela Kayombo ambaye pia ni mtumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe anayeishi na VVU tangu mwaka 1999
Baadhi ya watumishi wa halmashauri hiyo wakiwa katika foleni wakisubiri kupima afya zao wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo
KAMPENI ya kuhamasisha Upimaji wa Virusi vya Ukimwi mahali pa kazi imezinduliwa kitaifa mkoani Njombe huku baadhi ya watumishi wenye maambukizi hayo wakilalamika kutelekezwa.
Kauli Mbiu ya kampeni hiyo iliyoanza Septemba 23 na itakayofanyika hadi Desemba 1, mwaka huu inasema “mfanyakazi jitambue, pima mapema, epuka maambukizi mapya, ubaguzi na unyanyapaa, zuia vifo vitokanavyo na Ukimwi.”
Alipokuwa akiizindua kampeni hiyo Katibu Mkuu Utumishi, George Yambesi alisema kampeni hiyo inalenga kutoa msukumo wa utekelezaji wa mikakati ya kudhibiti Ukimwi kitaifa na kimataifa ili kufikia azma ya sifuri tatu.
“Sifuri tatu kwa maana ya maambukizi mapya sifuri, vifo sifuri na unyanyapaa sifuri ifikapo mwaka 2015,” alisema mbele ya wawakilishi wa mikoa ya Njombe na Iringa waliohudhuria uzinduzi huo.
Wakati mkoa wa Njombe unaongoza kitaifa kwa kuwa na asilimia 14.8 ya maambukizi, mkoa wa Iringa ni wa pili kitaifa kwa kuwa na asilimia 9.1 ya maambukizi.
Alisema kampeni hiyo inahimiza utekelezaji wa dhati wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) na maazimio yaliyowekwa kwenye Mkutano Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu UKIMWI uliofanyika mwaka 2001 Jijini New York, Marekani.
Mbali na Virusi vya Ukimwi (VVU), Yambesi alisema kwa kupitia kampeni hiyo watumishi na wananchi wengine watapata fursa ya kupima magonjwa sugu yasio ya kuambuzwa kama kisukari, shinikizo la damu, moyo, saratani, pumu na kupooza.
Alisema magonjwa hayo ambayo zamani yalikuwa yakihesabika kama magonjwa yanayowaathiri zaidi watu wenye uwezo mkubwa kiuchumi hivisasa yanaoonekana ni ya kawaida kwa watu wa kawaida.
Yambesi alisema kutopima afya kuna athari nyingi hasa kupungua kwa nguvu kazi, kuongezeka kwa gharama za matibabu na kupungua kwa tija inayoathiri ukuaji wa pato la taifa.
“Ili kuepuka matatizo hayo kuna kila sababu ya kuhamasiha watumishi wa umma kujali afya zao na kupima ili wachukue hatua kama wahenga walivyosema kinga ni bora kuliko tiba,” alisema.
Alisema katika kutekeleza ya wahenga ni muhimu kupima afya mara kwa mara kunasaidia kuepuka maambukizi mapya na wale wenye VVU kupunguza athari ya kuambukizi wengine,” alisema.
Alisema kwa takwimu za mwaka 2013, Tanzania ina  watumishi wa umma zaidi ya 500,000 ambao ni sehemu muhimu ya nguvu kazi ya taifa hivyo wanaohitaji kuwa na afya bora ili watekeleze wajibu wajibu wao.
“Tumekwisha weka misingi mizuri ya kulinda afya zetu kwa kuandaa waraka kuhusu Ukimwi na magonjwa sugu yasio ya kuambukizaa. Ni muhimu kwa taasisi za serikali kutekeleza maelekezo yote ili watumishi wa umma wawe ni wale wenye afya bora,” alisema.
Alisema watumishi wanapaswa kuwa wazi baada ya kugundulika na maambukizi ya VVU ili waweze kupata huduma muhimu ikiwemo ya matumizi ya dawa za kupunguza makali ya VVU (ARVs).
Watumishi wawili wa idara ya afya ya halmashauri ya wilaya ya Njombe wenye maambukizi ya VVU, Anjela Kayombo na Hilda Kapanda walisema pamoja na serikali kusisitiza mara kwa mara kuwasaidia watu wenye matatizo hayo, ahadi hiyo imeendelea kuwa hewa.
“Tunajua serikali inayo sera inayolenga kuwasaidia wenye VVU kwa dawa, lishe na vitu vingine, lakini sisi hatujawahi pata chochote,” alisema Kayombo.
Kampeni hiyo inafanywa kwa pamoja na serikali na Shirika la Kazi Duniani (ILO) ambalo katika uzinduzi huo liliwakilishwa na Getrude Sima ambaye ni Mratibu wa Ukimwi mahali pa kazi wa shirika hilo. (BONGOLEAKS)

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...