Skip to main content

TUPSE KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI WAPATA VIONGOZI WAPYA


https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14854029cf438802&attid=0.1&disp=inline&realattid=file1&safe=1&zw&saduie=AG9B_P9BRHotx0LdPyXvG8i9awjW&sadet=1410164085313&sads=_ppxmeBolFQN3MPur3RKQDkZfwA 
Katibu wa TUPSE Taifa, Edson Eliya Kivelege akiongea na waandishi wa habari muda mfupi wa kutangaza viongozi wa kanda ya nyanda za juu kusini cha chama hicho jana. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA


https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14854029cf438802&attid=0.2&disp=inline&realattid=file2&safe=1&zw&saduie=AG9B_P9BRHotx0LdPyXvG8i9awjW&sadet=1410164186242&sads=jZ2WXi29kqRrfuLXv7u-e1tt4Bg

Na Friday Simbaya, Iringa
Chama cha Wafanyakazi Walinzi Binafsi Tanzania (TUPSE) Kanda za Nyanda
za juu Kusini kimepata viongozi wapya watakao kuwepo madarakani kwa
kipindi cha miaka mitano, imefahamikia.

Akitangaza majina ya viongozi hao waliochaguliwa katika mkutano
uliofanyika jana Katibu wa TUPSE Taifa, Edson Eliya Kivelege
alimtangaza  Yareh Mazengo kuwa mwenyekiti wa kanda.
 Wajumbe waliochaguliwa kuunda Kamati Kuu ya Utendaji ni Haruna
Chalala na Selemani  Mkwawa, wajumbe wa Mkutano Mkuu Taifa
waliochaguliwa ni Lazaro Msangi, Tujia Nyamoga, Paulo Kaoyama na
Aloyce  Mwamakula na mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa wanawake
alichaguliwa Mwanne Ramadhani na Oliver Daniel  alichaguliwa kuwa
Kaimu Katibu Kanda za Juu Kusini.
Viongozi hao waliochuguliwa waliahidi kuchapa kazi kwa uweledi na kwa
ufanisi pamoja na kushughulikia changamoto mbalimbali zinazowakabili
wanachama.
Kivelege aliongeza kuwa Iringa ina jumla ya makampuni ya ulinzi
binafsi 36 nyingi zikitoka nje ya mkoa, lakini pamoja na hayo kampuni
zenye ofisi azizidi kumi (10) na kusababisha kukosa mawasiliano.
Alisema kuwa chama kinapotaka kuwasiliana na wanachama wake kinapata
shida ya kuonana na viongozi kwa ajili yakutatua kero za wanachama kwa
sababu ofisi nyingi za waajiri zipo Mbeya, Morogoro na Dar es Salaam.
Alisema kuwa kampuni nyingi hapa Iringa zinafanyakazi za  udalali kwa
sababu hiyo kampuni hizo zinakuwa zinawaajiri walinzi wasiokidhi
vigezo ambao wanakuwa na uweledi mdogo kuhusiana na masuala ya ulinzi.
"Kazi ya ulinzi ni kazi nyeti ambayo inahitaji mawasiliano ya wazi
kati ya mwajiri na mfanyakazi na mfanyakazi na mteja (watu
wanaowalindia mali) na chama cha wafanyakzi," alisema.
Aliongeza kuwa sare zinatakiwa kutolewa bure kwa walinzi na zitolewe
pea mbili kwa ajili ya kubadilisha na sehemu za baridi walinzi
wapatiwe makoti mazito.
Aliongeza kuwa walinzi wasipopatiwa mavazi na viatu kulingana na hali
ya hewa wanalazimika kutafuta mahala salama na kukoka moto na kulala
malindoni. Pia, alisema kuwa kampuni nyingi za walinzi hazitoi
mikataba kwa
wafanyakazi wala vitambulisho kwa walinzi ambapo inakuwa vigumu
kuwatambua walinzi pindi wanapopata matatizo.

Hata hivyo katibu mkuu huyo waliwataka waajiri kuwalipa nyongeza ya
mishahara kuanzia Juni 1, 2013 sawa na asilimia 46.4 ya kima cha chini
cha mshahara, kama ilivyotangazwa na serikali kupitia bodi ya
mishahara mwaka juzi.
Alitoa wito kwa waajiri pia kufuata utaratibu wa ulipaji wa mishahara
sio kila kampuni kuwa na tarehe yake ya kulipa mshahara na kuwataka
waajiri nchini kuwalipa wafanyakazi mapunjo ya mishahara yanayotokana
na kupandishwa kwa kima cha chini cha mishahara  kilichotangazwa na
serikali mwaka jana.
Walisema kuwa kumekuwepo na vitisho kutoka waajiri wao wanapogundua
kwamba wamejiunga vyama vya hiari na pamoja na kuanzisha matawi ya
vyama vya wafanyakazi.
Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...