Skip to main content

WANAFUNZI 21,540 KUFANYA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI MKOANI IRINGA

 Wanafunzi wa shule ya msingi chemchem katika Manispaa ya Iringa wakiwa juu ya paa la choo  wakisafisha  ikiwa ni sehemu ya maandalizi kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2014 mtihani huo utakaofanyika  tarehe 10 na 11/9/2014, ambapo shule za msingi 458 kati ya shule 484 ndizo zenyewanafunzi watakaofanya mtihani wakumaliza elimu ya msingi mkoani Iringa. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)

 https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=148551792f099bb1&attid=0.1&disp=inline&realattid=file0&safe=1&zw&saduie=AG9B_P9BRHotx0LdPyXvG8i9awjW&sadet=1410257157005&sads=8ez09vR2Miii--otw272s0xIDF8
Afisa Elimu Mkoa wa Iringa, Joseph Mnyikambi akiongea na waandishi wa habari leo ofisini kwaka. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)

Na Friday Simbaya, Iringa
Jumla ya wanafunzi 21,540 wakiwemo wavulana 9,779 na wasichana 11,761 ndio watakaofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka huu mkoani Iringa, imefahamika.

Mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2014 utafanyika  tarehe 10 na 11/9/2014, ambapo shule za msingi 458 kati ya shule 484 ndizo zenye wanafunzi watakaofanya mtihani wakumaliza elimu ya msingi.
Akiongea na waandishi wa habari leo, Afisa Elimu Mkoa wa Iringa,
Joseph Mnyikambi alisema idadi ya wanafunzi wanaofanya mtihani mwaka 2014 imepungua ukilinganisha na mwaka jana, 2013 ambapo kulikuwa watahiniwa 23,149 (wavulana 10,753 na wasichana 12,396) waliosajiliwa.
Afisa elimu huyo alisema maandalizi yote yamekamilika, kwani vifaa vyote vinavyohusiana na mtihani vimekwisha pelekwa kwenye halmashauri zote za Mkoa wa Iringa.
"Wito wangu kwa wazazi wote wenye watoto wanaosoma darasa la saba, wahakikishe watoto wao wanakwenda kufanya mtihani," alisema.
Aliongeza kuwa wanafunzi walio darasa la saba wahakikishe wanazingatia maelekezo watakayopewa na wasimamizi.
Mchanganuo kihamashauri ni kama ifuatavyo; Manispaa ya Iringa
waliosajiliwa mwaka huu ni 3,264, Halmashauri ya Iringa, 5,914, Kilolo, 5,142 na Mufindi wanafunzi waliosajiliwa ni 7,220.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...