Skip to main content

CCM IRINGA KWAJIPANGA KWA AJILI YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Katibu CCM Wilaya ya Mufindi Miraji Mtaturu
Katibu CCM Wilaya ya Mufindi Miraji Mtaturu kulia, akiwa na Mstahiki Meya Amani Mwamwindi (kushoto) na  katikati ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iringa Mjini Abed Kiponza.



Na Mathias Canal

Chama cha Mapinduzi (CCM) Iringa Mjini kimenufaika kisiasa baada ya juzi kupata wanachama wapya 110.

Wanachama hao vijana, baadhi yao wakitokea katika Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) cha mjini Iringa, walikabidhiwa kadi zao na kuapa kuwa waaminifu
katika chama hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa stendi ya mabasi yaendayo vijijini ya Mlandege.

CCM iliamua kuutumia uwanja huo kikilenga kupima mwitikio wa wanachama na wapenzi wake ikiwa ni takribani wiki moja tu tangu viongozi wa kitaifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) akiwemo Dk Wilbroad Slaa kufanya mkutano wao katika uwanja huo huo.(P.T)


Idadi ya watu waliojitokeza katika mkutano huo ilielezwa na Mwenyekiti wa CCM Manispaa ya Iringa, Abeid Kiponza kwamba ni ya kuridhisha pamoja na kwamba ulihutubiwa na viongozi wa mkoa na wilaya tofauti na ule wa Chadema uliohutubiwa na viongozi wa kitaifa.

Baada ya wanachama hao wapya kuapishwa, Katibu wa CCM wa Wilaya ya Mufindi, Miraji Mtaturu alikabidi Sh 500,000 kwa wanachama hao wanaounda tawi la VETA.

"Huu ni mchango wa CCM kwa tawi lenu jipya, kama mlivyoainisha kwenye risala yenu, ni matarajio yetu kwamba mtatumia fedha hizo kuanzisha shughuli itakayowahamasisha muwe wajasiriamali," alisema.

Pamoja na tawi hilo kuchangiwa Sh 500,000; tawi la CCM la Mlandege linaloundwa na madereva taxi nalo lilikabidhi na katibu huyo Sh500,000.

"Haya ndio mambo ya CCM, tunaisimamia serikali kutekeleza Ilani na wakati huo huo tunachangia shughuli za maendeleo za wadau wetu wote na wakati mwingine bila kujali itikadi za siasa, tumefanya hivyo sehemu nyingi na tutaendelea kufanya hivyo" alisema Mtaturu.

Mtaturu alisema siasa ni maisha ya watu na kwa kupitia Ilani ya CCM serikali imeendelea kuzipatia suluhu kero mbalimbali zinazowakabili wananchi.

Katika mkutano huo Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa, Amani Mwamwindi alielezea kazi mbalimbali zilizotekelezwa na halmashauri yake kupitia Ilani ya CCM.

"Tumefanya mengi katika sekta ya afya, elimu, barabara, umeme, maji, biashara, ujenzi na nyingine nyingi. Nyie ni mashahidi," alisema.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu alitoa ufafanuzi wa vifungu mbalimbali likiwemo suala la muundo wa serikali na sifa za kupata wabunge na mawaziri kupitia Katiba Inayopendekezwa.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...