Skip to main content

CHADEMA YAFUNIKA IRINGA MJINI

Dk Slaa mbele ya wafuasi wa Chadema wa Iringa Mjini katika mkutano uliofanyika Mlendege mjini Iringa
Sehemu ya vijana waliohudhuria
Akisisitiza jambo
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimefanya mkutano katika uwanja mpana wa stendi ya mabasi ya Mlandege, mjini Iringa; mkutano uliolezwa na wapekuzi wa mambo ya siasa wa mjini hapa kwamba umevunja rekodi ya mikutano yote iliyowahi kufanywa na chama hicho mjini Iringa.

Kwa kadri muda ulivyokuwa unazidi kwenda wapenzi na wasio wapenzi wa chama hicho waliendelea kumiminika katika stendi hiyo na kusikiliza kile kilichohotubiwa na baadhi ya viongozi wakuu wa chama hicho.

Mbali na  Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, mkutano huo ulihutubiwa na Katibu Mkuu wake, Dk Wilbroad Slaa, Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara, Profesa Abdalla Safari na Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu.

Wakati Mchungaji Msigwa alizungumzia mambo mbalimbali aliyofanya tangu alipochaguliwa kuwa mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini mwaka  2010, wengine wote walizungumzia uchaguzi wa mwaka huu wa serikali za mitaa na vijiji, uchaguzi mkuu wa mwakani na dhamira ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kukubaliana kusimamisha mgombea mmoja mmoja katika chaguzi zote zajazo.

Katika mkutano huo, Dk Slaa aliwataka wafuasi wa chama hicho kwenda kwa wenyeviti wa mitaa na vijiji kwa lengo la kuandikishwa katika daftari la kuandikisha wakazi wa kila kaya ndani ya kata.

Daftari hilo kwa mujibu wa Dk Slaa ndilo litakalotumika kwajili ya uchaguzi wa Desemba mwaka huu wa serikali za mitaa na vijiji.

“Ni haki ya kila mtanzania kuandikishwa katika daftari hilo. Daftari hilo sio la CCM wala la chama chochote, ni kwa ajili ya watanzania wote, kwahiyo akikisheni mnaandikishwa ili muwez kushiriki katika uchaguzi huo,” alisema.

Aliwasihi wafuasi wa chama hicho kutopuuza suala hilo kwani wakianya hivyo nafasi yao ya kushinda katika uchaguzi huo itakuwa ndogo.

“Kwahiyo msije mkajitokeza kuilalamikia CCM baada ya kuangushwa katika uchaguzi huo,” alisema.

Kuhusu Katiba
Dk Slaa alisema Ukawa watapita mtaa kwa mtaa na kijiji kwa kijiji pindi Katiba inayopendekezwa itakapopelekwa kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura.

“Hata ikiletwa kesho, hatuna shida, lakini CCM ni lazima wajue kwamba tutapita kila mahali kwa lengo la kuwahamasisha wananchi kuikataa,” alisema na kuongeza kwamba wanaikataa kwa kuwa haitokani na mapendekezo ya wananchi.

Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa mwakani
Dk Slaa alisema Ukawa wako katika hatua za mwisho za makubaliano ya kusimamisha mgombea mmoja mmoja katika chaguzi zote.

Hata hivyo alisema pamoja na makubaliano hayo kutakuwa na vigezo vitakavyotumiwa ili kuwapata wagombea safi .

“halitakuwa suala la kupeana tu, eti kwasababu tumekubaliana hivyo, ni lazima tupate wagombea wenye sifaili tuweze kukabiliana vizuri na CCM,” alisema.

Ili kufanikisha chaguzi hizo, chama hicho kilisema kinahitaji rasilimali fedha na ndipo ulipotolewa wito kwa wafuasi wake kuchangia kupitia mfumo wa simu za mkononi.

“Hatuhitaji fedha nyingi kutoka kwenu, tuchangieni Sh200, 300 au 500 ili zisaidia katika harakati za mabadiliko,” Dk Slaa alisema wakati Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu aliyewahi kufanya kazi na VODACOM akitoa maelezo ya namna ya kukichangia chama hicho kwa kutumia mitandao ya simu,” alisema. (BONGOLEAKS)

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...