Skip to main content

ITUNUNDU FC MABINGWA WA KOMBE LA SPANEST



Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Dk Leticia Warioba akimkabidhi kombe la ushindi wa ligi ya SPANEST, kapteni wa Itunundu Fc
Hapa akikabidhi cheti cha ushindi
Akiwavisha Itunundu FC medali za dhahabu
Akiwapa zawadi ya mpira miwili
Itunundu FC katika shamrashamra
Kapteni wa Kinyika FC akipokea zawadi ya mpira, cheti na Sh 200,000 taslimu
Alipokuwa akikagua timu
Timu zikionesha nembo ya ligi hiyo
KLABU ya Itunundu (Itunundu FC) imetwaa kombe la SPANEST, kitita cha Sh300,000, seti moja ya jezi, mpira mmoja, medali za dhahabu na cheti baada ya kuibwagwa kwa bao 1-0 Kinyika FC katika fainali za ligi hiyo zilizopigwa juzi kwenye uwanja wa Kimande Pawaga, Iringa Vijijini.
Kwa ushindi wa fainali ya ligi hiyo yenye kauli mbiu “Piga Vita Ujangili, Piga Mpira Okoa Tembo” inayolenga kuongeza mwitikio wa vijana katika harakati za serikali na wadau wake za kupambana na ujangili, Itunundu FC imepewa pia fursa ya kutembelea bure Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.
Bao hilo lililoizamisha Kinyika FC iliyoonekana kuutawala mchezo kwa karibu dakika zote za mchezo liliwekwa kimiani na mshambuliaji wa kati wa Itunundu FC, Siani Chambulika katika dk 39 ya kipindi cha kwanza.
Chambulika (18) alionekana shujaa mbele ya mashabiki zaidi ya 5,000 wa tarafa ya Idodi na Pawaga waliohudhuria fainali hiyo ya kwanza ya kombe hilo baada ya kupokea pasi kutoka kwa kiungo mshambuliaji Klopa Mtogesewa na kufanikiwa kuwaadaa walinzi wa Kinyika FC kabla ya kuachia shuti kali lililomshinda golikika wa Kinyika FC, Asid Samre na kuzama kimiani.
Pamoja na Kinyika FC kufanya mabadiliko matatu katika kipindi cha pili kwa kuwatoa Elisha Sila, Ramadhani Kapova na Jeremia Manga na kuwaingiza Robert Mahombero, Myagaro Mwiravi na Festo Savya, hawakufanikiwa kupenya ngome ya Itunundu FC.
Pamoja na kupoteza mchezo huo uliohudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Dk Leticia Warioba, Mwakilishi wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF), Elliud Mvella, madiwani, makaribu tarafa ya Idodi na Pawaga na wawakilishi wa SPANEST na Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa), Kinyika FC waliondoka na Sh200,000, cheti, medali za shaba, mpira mmoja na seti moja ya jezi.
Mshindi wa tatu, Kitisi FC alijinyakulia cheti na Sh 100,000 baada ya kuibwaga Kimande FC kwa bao 1-0. Zawadi zote kwa washindi zilikabidhiwa na Mkuu wa Wilaya ya Iringa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk Christine Ishengoma.
Ligi hiyo itakayokuwa ikichezwa kila mwaka inashirikisha vijiji 21 vinavyounda Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Tarafa ya Idodi na Pawaga (Mbomipa) inayopakana na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ambayo sehemu yake kubwa ipo wilayani Iringa.

Wapenzi wa soka watakaopenda kujumuika na timu Itunundu FC kujionea rasilimali mbalimali zilizoko katika hifadhi ya Ruaha, kwa mujibu wa Mratibu wa Spanest ambao ni Mradi wa Kuboresha Maeneo Yaliyohifadhiwa Kusini mwa Tanzania (SPANEST), Godwell Ole Meing’ataki watalazimika kuchangia Sh 25,000 kwa ajili ya usafiri wa kwenda na kurudi pamoja, chakula na tozo la kuingia katika hifadhi hiyo. (BONGOLEAKS)

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...