Skip to main content

Kinana awaasa makatibu wa CCM wa wilaya na mikoa

 
 
 
 
Joyce Kasiki, Dodoma

KATIBU mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Abdulrahaman Kinana amewaomba  makatibu wa CCM wa wilaya na mikoa nchini kufanya maandalizi mazuri kwa kuteua wagombea wazuri wanaokubalika,wanaopendwa na wanaoheshimika  katika jamii ili chama kiweze kushinda kwa kishindo katika chaguzi zijazo.

Kinana  alisema  hayo  mjini Dodoma wakati akifunga semina ya siku ya moja ya sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa na makatibu hao.

Alisema kuwa, tukishinda vizuri kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa watakuwa wamejenga msingi mzuri kwa ajili ya uchaguzi mwaka ujao ambapo ushindi huo huo utasaidia ushindi mwingine mkubwa zaidi wa madiwani,wabunge na rais mwaka ujao.

Vile vile alisema ,  yeye binafsi anaamini mwaka ujao pia ushindi ni kwa CCM kutokana na kazi nzuri inayofanywa na watendaji na viongozi wa chama na kuwaomba kujtahidi kadri ya uwezo wao kuongeza juhudi maarifa na ufanisi.

Kinana alisema   kuwa mwaka 2009 katika uchaguzi wa seriklai za mitaa ushindi wa CCM ulikuwa ni kwa asilimia 96 ambapo asilimia 4 zilizobaki waligawana vyama vya upinzani kama sehemu ya wao kupumulia hivyo anaamini hawatapata asilimia zaidi ya hizo walizopata.

Akielezea kuhusu ziara zake anazozifanya katika mikoa mbalimbali hapa nchini amesema ameridhishwa na maandalizi yaliyopo mikoani na wilayani hivyo hana sababu ya kutokuwa na imani kwamba ushindi kwa CCM utakuwa mkubwa sana.

Amesema mpaka sasa imebaki mikoa 8 ambapo mpaka mwezi februari mwakani atakuwa amemaliza mikoa yote nchini lengo likiwa ni kuimarisha chama, kusukuma,kusimamia, kuhimiza utekelezaji wa ilani na  ushindi katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...