Skip to main content

MWANRI: ZINGATIENI WELEDI WAKATI WA KUANDAA MAANDIKO YA MIRADI


 Kaimu Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (aliyesimama) akizungumza na baadhi ya viongozi waandamizi wizara za viwanda na biashara, fedha, uchukuzi, nishati na madini pamoja na viongozi waandamizi kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Zanzibar.  



 Bibi Maryam Khamis (Wapili kulia) Mtaalam wa uchumi kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Zanzibar akizungumza katika kikao hicho.

Mmoja wa wajumbe wa kikao hicho, Bw. Aunyisa Meena kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara akichangia mada.


Na Saidi Mkabakuli

Wapanga mipango nchini wameaswa kuzingatia weledi wakati wa kuandaa maandiko ya miradi yanayowasilishwa kwa wafadhili ili kuongeza ushindani dhidi ya nchi nyingine wakati wa uwasilishaji wa maombi ya kupatiwa ufadhili wa miradi ya maendeleo.

Wito huo umetolewa na Kaimu Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri wakati alipofanya mazungumzo na viongozi waandamizi kutoka wizara za viwanda na biashara, fedha, uchukuzi, nishati na madini pamoja na viongozi waandamizi kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Zanzibar.

Bibi Mwanri alisema kuwa kuna ushindani mkubwa kwa nchi zinazoomba ufadhili wa miradi ya maendeleo hivyo uandishi wa maandiko yenye kuzingatia weledi na viwango vya kimataifa ni msingi katika kuongeza ushindani na kuweza kuwashawishi wafadhili kuvutiwa na miradi husika.

“Katika kukabiliana na ushindani hatuna budi kujikita katika weledi na kuandika maandiko yenye kuweza kuvutia wafadhili ili waweze kuja kuwekeza nchini kwetu, ili tuweze kutimiza ndoto zetu za kuifanya Tanzania kuwa nchi yenye uchumi wa kati kufikia mwaka 2025” alisema Bibi Mwanri.

Mwezi Juni mwaka 2011, Serikali iliandaa Mpango wa Kwanza wa Maeneleo (2011/12 – 2015/16) kwa lengo la kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 ambapo Mpango huu ulihitaji takribani trilioni 40 ili kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo kwa kipindi cha miaka mitano.

Kwa mujibu wa Mpango huo, vyanzo vya utekelezaji wake ni  pamoja na Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP);  uwekezaji wa kigeni; Hati Fungani kwa Waishio Ughaibuni; Hatifungani za ndani; Hati Fungani katika Masoko ya Nje; Mifuko ya Pensheni na hifadhi ya jamii; na makubaliano ya ushirikiano wa kiuchumi wa nchi zinazoendelea.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...