Skip to main content

Tahliso:TCU simamieni majukumu yenu vizuri



Ofisa Habari wa Taasisi ya Vyuo vya Elimu ya Juu Tanzania (Tahliso), , Andrew Mwakalobo.PICHA: OMAR FUNGO

Jumuiya ya Wanafunzi wa Vyuo Vikuu (Tahliso) wameitaka Tume  ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kusimamia majukumu yake vizuri kwa vyuo ambavyo vinaongeza ada kinyume cha utaratibu.


Wamevitaja baadhi ya vyuo hvyo kuwa ni KCMC, CUHAS-Bugando na St. Francis Ifakara. Pia, Tahliso wameitaka TCU kuacha kuwatoza wanafunzi wa elimu ya juu Sh. 20,000 ikiwa ni mchango wa ‘Quality Assurance fee’ kwa madai ya kuendesha shughuli za TCU.

Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa Tahliso, Musa Mdede, alipozungumza kuhusu maazimio ya mkutano mkuu uliofanyika Septemba 25 hadi 27, mwaka huu mkoani Iringa. Alisema kumekuwa na malalamiko ya ongezeko la ada hadi kufikia Sh. milioni tano kutoka Sh. milioni tatu.

“TCU imekuwa haizungumzii au kuchukua hatua juu ya suala hili, kuna wanafunzi ambao wameshindwa kuendelea na masomo, tunatengeneza Taifa la wasio na elimu na kisha umasikini,” alisema Mdede.

Aliongeza kuwa mikopo inayotolewa na serikali ni asilimia 40 badala ya 100 kwa wanafunzi wa vyuo vikuu binafsi hususan fani ya afya na kusema vyuo vingi kwa upande wa ada na michango wanahitajika kulipa ada ya Sh. milioni tano hadi sita.

Hata hivyo Mdede alizungumzia utoaji wa mikopo kuzingatiwa pia na kwa wanafunzi wa elimu ya kati yaani Stashahada kutokana na wanaosoma katika fani ya uuguzi, udaktari, ufamasia, ugavi ndiyo wanaofanya kazi  pembezoni mwa nchi.

Tahliso imeitaka serikali kutoa kipaumbele kwa mikopo ya wanafunzi wa fani zote wa elimu ya juu kutokana na nchi kuhitaji wataalam wa nyanja zote. Kwa mujibu wa TCU, jumla ya waombaji mkopo ni 58,037 na bajeti ya serikali ilikuwa ni kutoa mkopo kwa wanafunzi 30,000 tu.
CHANZO: NIPASHE

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...