Skip to main content

WANACHADEMA WAANZA KUJITOKEZA KUGOMBEA UONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA

Frank Nyalusi Mwenyekiti wa ccm Wilaya ya Iringa akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano
Wananchi wakifuatilia mkutano kwa umakini.
Na Mathias Canal, Iringa

Diwani wa Kata ya Mivinjeni Frank Nyalusi (CHADEMA) amehamasisha wakazi wa kijiji cha Ifunda,Kata ya Ifunda, Wilaya ya Iringa, Mkoani Iringa, kujiandikisha katika daftari la mkazi ili waweze kupiga kura pasipo matatizo yoyote.


Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na wakazi wa kijiji hicho waliojitokeza kwenye mkutano huo ambao lengo la mkutano huo ilikuwa ni kutoa elimu kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Desemba 14 mwaka huu.

Nyalusi amewataka wapenzi wa CHADEMA kutoogopa kuchukua fomu kwani matatizo ya Ifunda yataweza kutatuliwa na viongozi makini ambao wanapatikana kwenye chama hicho.
Nyalusi amesema maisha ya mtanzania yanaendelea kudidimia huku akitoa mfano wa mahindi ambayo yanauzwa shilingi 25,000 kijini hapo huku miaka miwili iliyopita yalikuwa yanauzwa shilingi 70,000 kwa gunia.

"Hatuichukii CCM kwa sababu ya jembe na nyundo, bali tunaichukia CCM kwa sababu ya usanii wao," alisema Nyalusi.

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wameulalamikia uongozi wa kijiji kwa kutowasomea mapato na matumizi jambo ambalo linawafanya wananchi kutojua fedha zilizopo na matumizi yake kwa ujumla.

Aidha Nyalusi amewakumbusha wananchi kwamba wanapaswa kusomewa mapato na matumizi kwani hilo ni jambo la wazi na linahitaji kufanyika kila baada ya miezi mitatu.

Nyalusi alitumia nafasi hiyo kumpongeza Beatrice Miyamba, Mwenyekiti wa kitongoji cha Kibaoni B-Ifunda (CHADEMA) kwa kuamua kujitokeza kugombea nafasi ya uenyekiti wa kijiji cha Ifunda.

Akizungumzia maamuzi ya kugombea nafasi ya mwenyekiti wa kijiji Beatrice alisema anaamini atashinda na kushirikiana na wajumbe pamoja na mtendaji wa kijiji ambaye atakuwa chini ya mwenyekiti wa kijiji.

"Nimeumia sana kutokana na wananchi kuteseka kwa sababu ya daraja linalounganisha kijiji cha Iganga na Ifunda kwenda kijiji Utengilinyi ambapo fedha zilizopatikana ilikuwa ni shilingi milioni moja iliyotengwa na serikali ambayo inasemekana kuwa zimetumiwa na wachache ambao ni viongozi wa serikali." alisema Beatrice.

Beatrice alisema kuwa pamoja na kwamba familia anayotoka inaongozwa na CCM lakini ameamua kufanya mageuzi kwa kuachana na chama hicho kwa ajili ya kupambana na ufisadi ili kuwakomboa watu wa Ifunda na taifa kwa ujumla.

"Mimi nategemea ushindi lakini kama ikitokea nikashindwa sitegemei kulalamika wala kubadilika bali nitaonyesha ushirikiano na yule atakayeshinda," alisema Beatrice


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...