Skip to main content

KABATI ATAKA WANAWAKE WAJITOKEZE KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI








MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Iringa Ritta Kabati (CCM) amewakata wananchi kutokubali kudanganywa na vyama vya siasa vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA) juu ya katiba inayopendekezwa na badala yake kuungana na watanzania wapenda maendeleo kuikubali katiba hiyo muda utakapofika.



Mbunge alitoa kauli hiyo wakati wa semina elekezi kwa kina mama  wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Mufindi leo baada ya kufanya semina kama hizo katika wilaya ya Iringa na Kilolo.

Alisema kuwa semina ililenga kuwajengea uwezo wa kujiamini kwa wanawake waliojitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi wa serikali za mitaa na vijijini .


Kabati alisema kumekuwepo na upotoshwaji mkubwa ambao umeendelea kufanywa na UKAWA kwa kuzunguka huku na kule kujaribu kupotosha ukweli juu ya katiba iliyopendekezwa kwa madai kuwa ni katiba ya CCM na kuongeza  katiba hiyo ulifanywa na vyama vyote na makundi maalum.


Pia alisema kuwa kitendo cha baadhi ya wanasiasa wasilolitakia mema Taifa hili kwa kupotosha juu ya katiba hiyo ni sawa na kutaka kuona nchi haitawaliki na hivyo kuamua kuanza upotoshaji huo.


Alisema kuwa si kweli kama katiba hiyo iliyopendekezwa haina jambo lolote la msingi kama ambavyo UKAWA wamekuwa wakizunguka na kupotosha ila alidai kuwa ndani ya katiba hiyo kuna mambo mengi yamezingatiwa kwa ajili ya wananchi na Taifa kwa ujumla.


Akielezea kuhusu mchakato wa uchaguzi wa serikali za mitaa ,vijiji na vitongoji unaotaraji kufanyika hivi karibuni alisema kuwa upande wa mkoa wa Iringa wanawake baada ya kuhamasishwa wamejitokeza kwa wingi kuchukua fomu za kuwania nafasi mbali mbali za uongozi na kuwa baadhi ya maeneo wamepata kushinda kwa kishindo nafasi walivyoomba ndani ya CCM wakisubiri uchaguzi rasmi wa serikali .


Hivyo aliwataka wananchi wa mkoa wa Iringa kujitokeza kuwapa kura zao wanawake hao waliogombea nafasi mbali mbali na kuwa imani yake kuona kunakuwa na uongozi mchanganyiko.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...