Skip to main content

MWAKALEBELA AMWAGA VIFAA VYA MUZIKI OFISI YA CCM ...!

 
Kamanda wa UVCCM Wilaya Iringa mjini na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM, Frederick Mwakalebela (kushoto)  amekabidhi vifaa vya muziki vyenye thamani ya shilingi milioni nane (8m/-) kwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iringa mjini Abedi Kiponza (wa pili kushoto) na Katibu wa CCM Zongo Lobo Zongo (wa pili kulia) kwa ajili ya kusaidia shughuli za chama katika masuala ya kunadi sera na ilani ya uchaguzi ya mwaka  2010. Shughuli hiyo ilikwenda sambamba na kumuaga aliyekuwa mkuu wa mkoa wa iringa Dkt. Christine Ishengoma kichama ngazi ya wilaya.

 Kamanda wa UVCCM Wilaya Iringa mjini na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM, Frederick Mwakalebela akiongea na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kukabidhi vifaa vya muziki vyenye thamani ya shilingi milioni nane (8m/-) kwa ofisi kuu ya CCM Wilaya ya Iringa mjini leo. Alisema kuwa ameamua kusaidia vifaa vya muziki ili viweze ksaidia kunadi sera za chama katika kata zote ya Manispaa ya Iringa na hatimaye kupunguzu gharama kwa chama ya kukodi vyombo kama hivyo kwa gharama. Alisema kuwa badala hiyo pesa ya kukodi vyombo vya muziki hivyo itumike kwa shughuli nyinge ya kujenga chama.


Wanachama  wakishangilia kwa shangwe wakati wa hafla fupi ya kumuaga aliyekuwa mkuu wa mkoa wa iringa Dkt. Christine Ishengoma kichama ngazi ya wilaya, wilaya ya Iringa Mjini CCM akimtakia heri na safari njema aendako leo mchana katika ukumbi wa CCM Wilaya ya Iringa mjini. .

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt. Christine Ishengoma akifurahi jambo wakati wa hafla fupi ya kuagwa na wanachama wa CCM Wilaya ya Iringa Mjini na kuwaasa kuwa na mshikamano na upendo wa kutoka moyoni ilikuweza kupata ushindi katika chaguzi za serikali za mitaa na uchaguzi mkuu 2015. Hata hivo nafasi yake imechukuliwa na AminaJuma Masenza baada ya mabadiliko ya wakuu wa mikoa na wilaya yaliofanywa Rais Prof. Jakaya Kikwete hivi karibuni.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...