Skip to main content

NJIA BORA YA KUOKOA MAISHA YA WATOTO NA JAMII NI KUNAWA MIKONO











Kilele cha maadhimisho ya siku ya choo duniani, siku ya unawaji mikono na wiki ya usafi Tanzania imefikia kikomo ambapo zaidi ya watu bilioni 4.5 tu ndio wanaomiliki na kutumia vyoo bora huku watu bilioni 2.5 duniani kote hasa maeneo ya vijijini hawana vyoo bora.



Katika hotuba ya Katibu tawala wa mkoa wa Iringa, iliyosomwa na Mganga mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt Robert Salim, ya kufunga maadhimisho hayo Kimkoa iliyofanyika Kijiji cha Ifunda, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa mwaka 2013 umoja wa mataifa ulipitisha tarehe 19 Novemba ya kila mwaka kuwa ni siku rasmi ya maadhimisho ya choo Duniani, ambapo mwaka huo huo Tanzania ilipitisha rasmi tarehe 13-19 Novemba kuwa ni wiki ya usafi Tanzania pamoja na siku ya kunawa mikono Duniani sambamba na siku ya choo Dunia.




Taarifa zinaonyesha kuwa matumizi ya choo bora na kunawa mikono kwa sabuni ni moja ya njia bora ya kuokoa maisha ya watoto na jamii nzima kwa ujumla, kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni kupunguza kuenea kwa magonjwa ya kuhara na manufaa yake ni ya muda mrefu kwa afya na ustawi wa watoto na jamii kwa ujumla.



Takwimu zinaonyesha kuwa matumizi ya choo bora hupunguza magonjwa ya kuhara kwa asilimia 32 na kunawa nikono kwa sabuni hupunguza magonjwa hayo kwa asilimia 50, ambapo Takwimu za mwaka 2013 zinaonyesha kuwa watoto 1000 wanakufa kwa kila siku moja duniani kote kutokana na magonjwa ya kuhara.


Aidha baadhi ya taasisi zilipatiwa zawadi mbalimbali kutokana na uboreshaji wa huduma za maji, afya na mazingira ikiwa ni pamoja na shule ya msingi Nyololo, ambapo Manispaa ya Iringa ilipata zawadi ya kuweza kudhibiti uchafuzi wa mazingira katika maeneo ya mkusanyiko, huku Kitongoji cha Mpwapwa kilichopo kijiji cha Kihanga kilipata zawadi ya kuwa kitongoji kisichotupa kinyesi ovyo.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...