Skip to main content

TRA IRINGA KUFUATILIA MATUMIZI YA MASHINE ZA EFD

Meneja wa TRA Mkoa wa Iringa, Rosalia Mwenda
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Iringa itaendelea kufuatilia kwa karibu matumizi ya mashine za kielektoniki za kutolea risiti kwa wafanyabiashara wa mkoani hapa wanaotakiwa kwa mujibu wa sheria kutumia mashine hizo.

Wafanyabiashara hao kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Menejea wa TRA Mkoa wa Iringa, Rosalia Mwenda ni pamoja na wale waliosajiliwa kwa ajili ya kukusanya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na wale wa awamu ya pili ambao mauzo yao kwa mwaka ni Sh Milioni 14 na zaidi.

Akizungumza na wanahabari kuhusu maadhimisho ya nane ya siku ya mlipa kodi (Novemba 11-21, 2014), Mwenda alisema wakati wafanyabiashara 533 wamesajiliwa kwa ajili ya VAT, wengine 1,240 wamesajiliwa awamu ya pili ya matumizi ya mashine hizo baada ya kutambuliwa kuwa na mauzo ya zaidi ya Sh Milioni 14 kwa mwaka.

“Katika awamu hii ya pili lengo letu ni kuandikisha zaidi ya wafanyabiashara 5,000; kumekuwepo na changamoto katika kufikia lengo hilo, pamoja na hayo yote tunaendelea na kazi hiyo ili tufikie lengo hilo,” alisema.

Alitaja moja ya changamoto iliyosababisha wasifikie lengo hilo kuwa ni pamoja na kuendelea kwa migomo ya baadhi ya wafanyabiashara walioko katika awamu hiyo ya pili ya kununu na kutumia mashine hizo.

“Wakati wafanyabiashara hao wanapinga kutumia mashine hizo, baadhi ya wale walioko katika kundi la VAT hawatumihi ipasavyo mashine hizo,” alisema.

“Tunapoadhimisha  siku ya mlipa kodi ujumbe wetu kwa walipakodi wetu ni kuakumbusha kaulimbiu ya Risiti ni haki yako, asiyetoa anakwepa kodi,” alisema.

Akizungumzia hali ya makusanyo ya kodi katika kipindi cha 2013/2014, Mwenda alisema mkoa wa Iringa ulipangiwa kukusanya jumla ya Sh 37,575,300,000 hata hivyo haukuweza kufikia lengo hilo baada ya kukusanya Sh 35,845,879,036 ambayo ni sawa na asilimia 96.

Akiwasihi wapiga kura wa mkoani hapa, Afisa wa TRA mkoani hapa anayehusika na elimu kwa walipa kodi, Faustine Masunga alisema; “Watu wasiwaogope maafisa wa TRA na wala wasiogope au kukwepa kulipa kodi kodi kwasababu bila kodi nchi haiwezi kutekeleza mipango yake.”

Alisema TRA ilianza kusheherekea siku ya mlipakodi mwaka 2006 kwa lengo la kuwatunukua walipakodi ambao wapo mstari wa mbele katika kuweka kumbukumbu zao za biashara:

“Wanaolipa kodi zinazolingana na biashara zao, wanaojituma kulipa kodi kwenye tarehe zinazokubalika kisheria na wale wanaolipa kodi zao kwa hiari.


Masunga alisema kilele cha maadhimishi ya wiki hiyo ya mlipa kodi kitafanyika katika ukumbi wa IDYDC, Novemba 21, mwaka huu. (BONGO LEAKS)

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...