Skip to main content

BOMA LA MJERUMANI KUJENGWA MAKUMBUMSHO YA KISASA

CHUO Kikuu cha Iringa (UOI) kupitia mradi wa kuendeleza utamaduni nyanda za juu kusini uitwao Fahari Yetu (Southern Highlands Culture Solutions) kinatarajia kuanza ukarabati wa jingo la kale lilojengwa na serikali ya Ujerumani enzi za ukoloni 'Boma' mkoani Iringa.


Mradi huu wa kitalii ambao ni wa mamilioni ya shilingi za kitanzania utahusisha ukarabati, uhifadhi na uhuishaji wa iliyokuwa boma ya Iringa enzi za utawala wa kijerumani.


Akizungumza na waandishi wa habari jana naibu makamu mkuu wa chuo Dr. Hosea Mpogole kwa niaba ya kikuu cha Iringa zamani Chuo Kikuu cha Tumaini Profesa Nicholas Bangu alisema makubumsho ni kati ya maeneo bora kabisa duniani ya kujifunzia, kufanya maonyesho ya mambo ya kisayansi kama uvumbuzi, kazi za sanaa na za kihistoria na pia ni kituo muhimu kwa ajili ya utafiti, matamasha ya asili na ushawishi.


Alisema kwamba chuo kikuu cha Iringa kimejikita katika kutoa uwezo wa kitaaluma ambao utatoa fursa ya kufundisha kwa vitendo badala ya kuwa na nadharia pekee.


"Mradi huu wa Fahari Yetu umetenga fedha kwa ajili ya ukarabati ambao pia itaibadilisha Boma hili na kulifanya kuwa jingo la makumbusho ya urithi wa kiutamaduni. Mradi huu makao makuu yake yatakuwa chuo kikuu cha Iringa utafanya kazi kwa kushirikiana na wizara ya maliasili na utalii idara ya mambo ya kale, makumbumsho ya taifa, na ofisi ya mkuu wa mkoa Iringa ambao wote ni wadau wa Fahari Yetu," alisema Dr. Mpogole.


Dr. Mpogole pia alisema chuo kinapitia upya na kuboresha mtaala wake wa idara ya utamaduni na utalii (Cultural Anthropology and Tourism) ili kuboresha kozi hiyo na utafiti katika kuhakikisha kuwa taaluma inaunganisha shughuli za urithi wa mambo ya asili, utamaduni na uhifadhi kwa ajili ya kukuza sekta ya utalii nyanda za juu kusini na taifa kwa ujumla.


Dr. Mpogole aliongeza kuwa jengo la makumbumsho hilo ambalo hapo awali lilikuwa ni ofisi ya mkuu wa wilaya Iringa, litaleta manufaa katika kukuza na kuendeleza sekta za wajasiliamali wadogowadogo ambao moja kwa moja watahusiana na utalii wa kitamaduni.


Naye Katibu wa tawala wa mkoa wa Iringa, Ayub Wamoja kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Juma Masenza alisema kuwepokwa makumbumsho ndani ya mkoa kutakuza kwa kiwango kikubwa sekta ya utalii ndani ya nchi kwa kuongeza thamani ya vivutio.


Na pia kuwafanya watalii kukaa muda mrefu ndani ya nchi na hatimaye kuliongezea taifa pato.


Alisema matokeo la ongezeka la watalii ni pia ongozeko la ajira kwa mtu mmoja mmoja na hata sekta mbalimbali zinazojishughulisha na utalii hasa pale wajasilamali watakapoona fursa za uwekezaji katika tasnia ya utalii na utamaduni.


Katibu tawala huyo alisema kuwa nyanda za juu kusini zimebarikiwa kuwa na urithi mkubwa wa mali asili na utamaduni, hata hivyo bado urithi huu hajatumika ipasavyo ili kuweza kuchangia katika kukuza maisha ya jamii kutokana na ukosefu wa ufahamu bora miongoni mwa mwanajamii juu ya umhimu wa urithi wa utamaduni.


Alisema jengo hilo la kisasa la makumbumsho litakuwa katika iliyokuwa Iringa boma, jengo ambalo lilinjengwa na na utawala wa kikoloni wa kijerumani litatumika kwa ajili ya kuonesha mambo ya urithi wa kihistoria na kuvitia watalii duniani kote kuja kutembelea mkoa wa Iringa na vivutio vyake.


Hata hivyo ofisi ya mkuu wa mkoa, halmashauri ya Iringa, Manispaa ya Iringa, Makumbusho ya taifa, na Chuo Kikuu cha Iringa ndio washirika wakuu wa mradi wa Fahari Yetu-Southern Highlands Cultural Solutions kwa ufadhili wa Jumuiya ya Ulaya (EU).

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...