Skip to main content

BROADCAST WAREHOUSE YA UINGEREZA KUSAIDIA COMNETA

DSC_0220
Mwenyekiti wa mtandao wa vyombo vya habari vya kijamii Tanzania (COMNETA) ambaye pia ni Mkurugenzi wa redio FADECO ya wilayani Karagwe, Bw. Joseph Sekiku, akimtambulisha mgeni kutoka nchini Uingereza kwa wamiliki wa redio za jamii katika mkutano uliojadili masuala ya kiufundi uliofanyika mwishoni mwa juma Chuo kikuu huria.(Picha zote na Zainul Mzige).

Na Mwandishi wetu

Kampuni Broadcast warehouse ya Uingereza imesema ipo tayari kusaidia radio za jamii ambazo kwa sasa zinakabiliwa na changamoto nyingi za uendeshaji hasa katika masuala ya kiufundi kwenye teknolojia ya utangazaji ya digitali.


Mtaalamu wa kampuni hiyo, Brendan Lofty ambaye aliwasili nchini kwa ajili ya mkutano na wanachama mtandao wa vyombo vya habari vya kijamii Tanzania (COMNETA) amesema ipo haja ya kuangalia mfumo wa pamoja wa kiufundi ambao utafanya redio hizo kuwa endelevu.

Alisema anafahamu umuhimu wa radio hizo za jamii ambazo zinaelekeza nguvu kushughulikia matatizo ya jamii kuliko redio za biashara na kusema yupo nchini kuhakikisha anajibu kiu ya wamiliki hao inamalizika na wanaendelea na majukumu yao.

DSC_0246
Pichani juu na chini ni baadhi ya wanachama mtandao wa vyombo vya habari vya kijamii Tanzania (COMNETA) ambao ni mameneja na wamiliki wa redio za jamii nchini waliohudhuria mkutano wa siku moja uliojadili masuala ya kiufundi uliofanyika mwishoni mwa juma Chuo kikuu huria.

Alisema katika kuelekea uchaguzi na hasa baada ya TCRA kutoa hadidu za kuzingatiwa inafaa wahusuka wote kuwa katika hali ya kujiamini kwa kuwa na utaalamu unaotakiwa katika kuendesha redio hasa masuala ya kiufundi.

“Nimekuja kuwatoa hofu, tutaelezana na kushauriana namna bora ya kusaidiana kufikia kuwa na redio bora” alisema Lofty.
Alisema katika utafiti wake amebaini kwamba radio za jamii nchini zina kazi kubwa na ya maana kuliko zile za kibiashara na kwamba zipo zenye hali bora zaidi kiufundi kuliko zilizopo Ulaya.

DSC_0239
Naye Mwenyekiti wa Comneta, Joseph Sekiku akielezea mkutano huo amesema umeitishwa makusudi kwa ajili ya kupata uzoefu wa mtaalamu huyo wa Uingereza kutokana na redio nyingi kuwa na matatizo ya kiufundi kwenye digitali .

Alisema kutokana na makampuni yaliyouza vifaa mengi kutokuwa na program za kufuatilia vifaa vyao, redio nyingi zimejikuta zikilazimika kununua vifaa vingine walivyonavyo vinapopata hitilafu na hivyo kuongeza mzigo wa uendeshaji.

DSC_0262
Alisema wakati Comneta inataka kuwa na uwiano wa ubora wa vifaa na wauzaji wake wameona ni vyema kumuita mtaalamu huyo wa Uingereza ambaye pia kampuni yake inauza vifaa vya radio na digitali kuona namna bora ya kushirikiana.

Aidha alisema hali hiyo imesababishwa na mahitaji halisi ya kuzifanya redio hizo kuwa endelevu na kuendelea kuhudumia jamii hasa kuelekea katika uchaguzi.

Alisema nyingi ya radio hizo hazinahifadhi ya vitu vinavyorushwa kwa siku, hivyo kama masuala hayo yakitatuliwa suala la kufuatilia haki katika mashauri na TCRA yanaweza kuwa na nafuu zaidi.

DSC_0275
Mtaalamu kutoka kampuni ya Broadcast warehouse ya Uingereza, Bw. Brendan Lofty, akifafanua masuala ya kiufundi yanayohusu redio na programu zake kwa ujumla kwenye mkutano wa siku moja na wanachama wa COMNETA.

DSC_0293 DSC_0238
Meneja wa kituo cha redio jamii TUMBATU FM, Bw. Ali Khamis akielezea changamoto mbalimbali za kiufundi wanazokumbana nazo kwenye kituo chake wakati wa mkutano huo na Mtaalamu wa Kampuni ya Broadcast warehouse ya Uingereza, Bw. Brendan Lofty (hayupo pichani).

DSC_0233
Mkurugenzi wa redio jamii Uvinza Fm, Alhaji Ayubu Kalufya akiuliza swali kwa mtaalamu huyo Bw. Brendan Lofty(hayupo pichani).

DSC_0268
Mtaalamu kutoka kampuni ya Broadcast warehouse ya Uingereza, Bw. Brendan Lofty akibadilishana mawazo na baadhi ya wanachama wa mtandao wa vyombo vya habari vya kijamii Tanzania (COMNETA) wakati wa mkutano huo wa siku moja uliofanyika Chuo Kikuu Huria mwishoni mwa juma. (EDITED BY FRIDAY SIMBAYA)

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...